'CHAPO' KUFANYA UCHAGUZI MDOGO ASUBUHI HII
NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANACHAMA wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’ asubuhi hii ya August 31, 2024 wanatarajia kuingia kwenye zoezi la uchaguzi mdogo wa kumchagua Mkurugenzi wao mpya. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi huo Mwanasheria Siti Habib Mohamed, alisema tayari maandalizi yote ikiwemo utoaji wa fomu, maandalizi ya kura yameshakamilika. Alisema, hadi Augost 29 ambayo ilikuwa ndio siku ya mwisho ya uchukuaji na urejeshaji wa fomu, kulikuwa na mwanachama mmoja pekee, aliyechukua fomu hiyo. Alisema, tayari dirisha la zoezi hilo, limeshafungwa tokea Augost 29, majira ya saa 8:30 jioni, hivyo tayari kamati yake, imeshaliratibu zoezi hilo, linalitarajiwa kufanyika ofisi ya CHAPO Chake chake asubuhi ya leo. Alieleza kuwa, kwa upande wao, kila kitu kimeshakamilika, na lililobakia kwa sasa ni kuwasubiri wanachama, ambao ndio wapiga kura, kuteleleza wajibu wao. ‘’Kwa upande wa kamati yangu ndo...