Posts

Showing posts from October, 2025

WAGOMBEA CCM JIMBO LA CHAKE CHAKE, KUANZISHA WIKI YA MSAADA WA KISHERIA

Image
    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MGOMBEA Ubunge na Uwakilishi jimbo la Chake chake, wamesema kama wakipata ridhaa ya wananchi, wataanzisha wiki ya msaada wa kisheria jimboni humo, ili kuwasaidia wananchi, wenye changamoto za kisheria.   Walisema, wanayodhamira ya dhati kuhakikisha wananchi wa jimbo hilo, wanaondokana na changamoto za kisheria, kwa kuanzisha wiki ya msaada wa kisheria, kila baada ya muda.   Wakizungumza na baadhi ya watendaji wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’, wakati walipofika ofisini hapo, walisema wanachosubiri ni ridhaa tu ya wananchi.   Wagombea hao walisema, wamebaini kuwa, ipo haja ya kuongeza nguvu ya kutoa elimu, msaada na ushauri wa kisheria kwa wananchi, na hilo litawezekana kwa kuanzisha wiki ya msaada wa kisheria.   Mgombea Uwakilishi Abdulla-wahabi Said Abubakar, alisema kwa kushirikiana na viongozi wenzake, na baada ya kukaa na uongozi wa ‘CHAPO’, azma hiyo wanayo. ...

BODI CHAPO YANG'AKA UTORO, UVIVU WA WASAIDIZI WA SHERIA

Image
  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WAJUMBE wa Bodi wa Jumuiya ya Wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’, wamesema hawataki kusikia tena kuwa, wapo wasaidizi wa sheria, wamekuwa wavivu wa kufanya wajibu wao na kudharau vikao vinavyoitwishwa. Walisema, kila mmoja anajua kuwa, CHAPO kama ilivyo wa jumuiya nyingine, ni eneo la kujitolea, sasa kama wako tayari kuendelea nayo, wahakikishe wanaendelea kuwahudumia wananchi. Mwenyekiti wa Bodi hiyo Safia Saleh Sultan, alisema wakati wanaomba kuingia kwenye sekta ya wasaidizi wa sheria, suala la kujitolea na kujitoa, ndio kigezo kikuu. Alieleza kuwa, leo anashangaa kusikia kuwepo wasaidizi wa sheria ndani ya ‘CHAPO’, wamekuwa wavivu wa kutoa elimu na msaada wa kisheria kwa jamii. Alifahamisha kuwa, uvivu wao wa kufanyakazi na jamii, inaweza kupoteza mwelekeo kwa wananchi, na kuiangusha CHAPO, jambo ambalo akiwa Mwenyekiti, hataki kulisikia. ‘’Kila mmoja kuanzia sasa afanye wajibu wake, ambao ni kutoa elimu, ushauri na...