‘’MLIOPEWA MAFUNZO WA SHERIA WAWI WAHAMASISHENI WANANCHI KUDAI HAKI ZAO’' CHAPO
NA MARYAM SALUM, PEMBA@@@@ KAIMU Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba, ‘CHAPO’ Kassim Ali Omar, amewataka wahitimu wa mafunzo ya sheria, kutoka shehia ya Wawi, kuwahamasisha watu kudai haki zao mbali mbali. Wito huo aliutoa leo Juni 19, 2023 Vikutani shehiani humo, kwenye ufungaji wa mafunzo ya siku ya tano, ya sheria kwa wajumbe wa kamati ya sheha na kamati nyengine, za shehia ya Wawi. Alisema, anaamini kwa mafunzo hayo, washiriki hao watakuwa waalimu wazuri kwa wenzao, katika kuwahamasisha kudai haki zao mbali mbali badala ya kuwakatisha tamaa. Alieleza kuwa, ndani ya mafunzo hayo wamejua mambo ambayo yanaweza kusababisha kesi kufutwa, kuondolewa au mtuhumiwa kutumikia kutiwa hatiani. ‘’Mimi naamini kwa mafunzo haya mliopewa ya sheria ngazi ya shehia, mtakuwa na uwezo kuwahamasisha wale waliokata tamaa, kwenda kudai haki zao, mbali mbali,’’alieleza. Katika hatua nyingine, Kaimu Mwenyekiti huyo wa Bodi ya wadha...