Posts

Showing posts from May, 2024

ZIARA YA ‘CHAPO’ YAFUFUA BARAZA LA WATOTO CHANJAANI

Image
    NA MWANDISHI MAALUM, PEMBA@@@@ UONGOZI wa shehia ya Chanjaani wilaya ya Chake chake Pemba, umesema ujio wa wasaidizi wa sheria kutoka Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilayani humo, umewasaidia kutambua dhana ya baraza la watoto kisheria, kinyume na hapo awali.   Hayo yameelezwa juzi na Sheha wa Chanjaani Khatib Ali Vuai, wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi, baada ya kumalizika kwa kikao, kilichojumuisha wasaidizi wa sheria, wajumbe wa sheha na askari shehia na kufanyika Chanjaani Gereji.   Alisema, hapo awali hakuwa na uwelewa mpana, wa nini maana ya baraza la watoto, utataratibu wake, aina ya wajumbe, idadi, kazi zao, utambuzi wake kisheria, ingawa ujio wa wasaidizi wa sheria umemfungua macho.   Alieleza kuwa, alikuwa anasikia tu ndani ya shehia yake, kuwa kuna baraza la watoto, ingawa alidhani ni suala lisilotambuliwa kisheria, na hakuwa na hamu ya kulifuatilia kwa undani.   Alifahamisha kuwa, kikao hicho cha wasaidizi wa s...

WEPO, CHAPO: 'MKIFAUATA NJIA HIZI MIGOGORO YA ARDHI KWISHA KAZI'

Image
  NA MWANDISHI WETU, PEMBA@@@@ WANANCHI kisiwani Pemba, wametakiwa wasikurupuke wakati wanapotaka kununua ardhi, na badala yake, wajiridhishe kwanza juu ya uhalali, wa umiliki kwa muuzaji, ikiwa ni njia moja wapo ya kuepusha migogoro, isiyokuwa ya lazima.   Hayo yameeleza leo Mei 21, 2024 na wasaidizi wa sheria kutoka Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Wete Pemba ‘WEPO’   na wenzao kutoka Jumuiya ya Wasaidizi wa sheria Chake chake ‘CHAPO’, wakati wakitoa elimu ya sheria, juu ya njia za kujiepusha na migogoro ya ardhi, kupitia kituo cha redio Istqaama kisiwani Pemba.   Walisema, wapo wananchi wamekuwa wakikubali kuuziwa ardhi kinyemela, pasi na mnunuzi kujiridhisha juu ya umiliki wa ardhi hiyo, kabla ya kuanza mchakato huo.   Walieleza kuwa, ili kujiepusha na migogoro ya ardhi, hakuna budi kwa mnunuzi, apate uthibitisho kutoka kwa muuzaji, kama vile nyaraka za matumizi ya ardhi, urithi, huba, kuvunja pori ambapo nyaraka hizo zitakuwa ni sehe...

CHAPO: YAWAPA MBINU WANAFUNZI WESHA KUKOMESHA UDHALILISHAJI

Image
  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@   WANAFUNZI wa Almadrssatul Fatuhu-l-khair ya kijiji cha Mchochani shehia ya Wesha, wilaya ya Chake chake Pemba, wametakiwa kuwaripoti waalimu, wazazi, kaka, wajomba na watu wengine maarufu, ikiwa watawagundua   wameanza mchezo wa kutaka kuwadhalilisha.   Ushauri huo umetolewa  leo Mei 19, 2024 na wasaidizi wa sheria shehia ya Wara Sabahi Mohamed Abdalla na mwenzake wa Wesha Khadija Said Khalfan, wakati wakitoa elimu ya kisheria, kuhusu viashiria vya udhalilishaji kwa wanafunzi hao, kwenye mkutano wa wazi ulioandaliwa na Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake ‘CHAPO’.   Walisema, wasijaribu kuwaficha watu wa aina yoyote, ikiwa watawabaini wameanza tabia ambayo, sio ya kawaida, kama vile kuwachezea sehemu zao za siri, hivyo wasisite kutoa taarifa.   Walieleza kuwa, katika hilo waondowe woga na wasiwasi, kwani sheria zipo kwa ajili ya kuwalinda, hivyo kama watahisi kuna mchezo wanachezewa, wasisi...

CHAPO YAANZA MAANDALIZI WAWI UANZISHWAJIA KLABU YA KUPINGA UDHALILISHAJI BARAZA LA WATOTO

Image
  NA ASHA ABDALLA, PEMBA@@@@              JUMUIYA ya wasaidizi washeria wilaya ya Chake chake Pemba, ‘CHAPO’ imesema inampango wa kuanzisha klabu maalum ya kupinga vitendo vya ukatili na udhalilishaji ndani ya baraza la watoto la shehia ya Wawi, kwa lengo la kulijengea uwezo, ili kutambua viashiria ya vitendo hivyo.      Hayo yameelezwa wasaidizi washeria wa shehia za Wawi, Wesha, Waram Mgogoni na Kibikoni wilayani humo, wakati wakizungumza na wajumbe wa baraza hilo, kwenye mkutano maalum wa wazi, wenye lengo la kupanga mikakati ya kutokeza vitendo hivyo.   Walisema kuwa CHAPO, inalojukumu kubwa la kuhakikisha kila shehia ya wilaya ya Chake chake, imefikiwa na elimu inayostahiki katika kupinga vitendo vya ukatili na udhalilishaji kwa watoto, ikiwemo kuanzisha klabu hizo.   Mmoja kati ya wasaidizi wa sheria hao kutoka shehia ya Wesha, Khadija Said Khalfan, alisema kuwa, wasaid...