‘CHAPO’ YAWAKOSHA WANANCHI KILINDI ELIMU YA SHERIA
NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI wa kijiji cha Kuungeni shehia ya Kilindi wilaya ya Chake chake Pemba, wamesema mfumo uliofanywa na Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’ kuwafuata kijijini kwao na kuwapa elimu ya kisheria, inafaa kuendelezwa. Walisema, mfumo huo unafaa kuendelezwa na kuwa imara zaidi, kwani umewasaidia katika kukuza uwelewa wao, hasa masuala la haki na fursa zao kisheria. Wakizungumza kwenye mkutano wa wazi, uliofanyika Mei 14, 2023 kijijini hapo, walisema wamepata uwelewa wa mambo kadhaa, ikiwa ni pamoja na maana ya wizi kisheria. Wananchi hao walisema, wamejua njia ambazo mwananchi anaweza kuingia kwenye kosa la wizi, ikiwa ni pamoja na kununua vifaa vya wizi, kuficha taarifa pamoja na kumpa mawasiliano. Mwananchi Massoud Juma Khamis, alisema ujio huo wa watendaji wa CHAPO, umewaamsha katika ufahamu pia wa masuala ya udhalilishaji, ule ambao sio maarufu kwa jamii. Alieleza kuwa, kutopeleka huduma za kibinadamu ambazo...