Posts

Showing posts from September, 2025

‘CHAPO’ YATIMIZA AHADI KWA WANAMICHEZO WAWI

Image
  NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@   WANAMICHEZO shehia ya Wawi wilaya ya Chake chake, wametakiwa kujiepusha na matumizi ya vilevi kama vile dawa za kulevya, kwani kufanya hivyo, wanaweza kuzima ndoto zao mapema kwenye michezo. Ushauri huo umetolewa na Msaidizi wa sheria wa shehia hiyo Fatma Hilali Salim, Septemba 9, 2025 shehiani humo, wakati akizungumza na wanamichezo hao na wananchi wingine, kwenye hafla ya kukabidhi mipira, iliyotolewa na Mkurugenzi Idara ya Katiba na Msaada wa sheria pamoja na Katib Mtendji wa Baraza la Vijana Zanzibar. Alisema, moja ya njia nyepesi kwa mwanamichezo yeyote ili asifikie ndoto zake kwenye michezo, ni matumizi ya dawa za kulevya, ambazo ni hatari kwa afya yake. Alieleza kuwa, dawa za kulevya sio tu kwamba zinazima ndoto kimichezo, lakini zinamshushia heshima, kutoonekana binaadamu kamili, kutoaminika katika jamii yake. ‘’Dawa za kulevya kwa mwanamichezo ni sumu ya kutokusonga mbele, maana hao munaosiki ni wachezaji wakubwa, walianza kuwa ...

WASAIDIZI WA SHERIA WAWAREJESHA WANAFUNZI WATORO MASOMONI

Image
  NA MWANDISHI WETU, CHAPO@@@@ FAMILIA mbili za shehia za Gombani na Ziwani wilaya ya Chake chake, wamewashukuru wasaidizi wa sheria wilayani humo, kwa kufanikiwa kuwarejesha watoto wao masomoni, baada ya kukatisha kwa zaidi ya miezi minne. Walisema tayari walishashindwa kuwanasihi na kuwatisha watoto wao ili kurejea masomoni, ingawa hawakufanikiwa, na kuamua kuwatafuta wasaidizi hao wa sheria. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa nyakati tofauti wazazi hao, walisema walitumia mbinu kadhaa ikiwemo kuwapeleka kwa askari wa ulinzi shirikishi, ingawa hakuwafanikiwa. Walisema, waliwatumia askari wa shehia ili kuwanasihi na kisha kuwatisha, ingawa walikuwa wanarejea masomoni kwa muda, kisha kuatisha tena. Mzazi Hassina Khamis Said, alisema aliamuwa kuwatafua wasaidizi wa sheria na haraka walifika kijijini kwao Semeweni, shehia ya Ziwani na kuwakabidhi kijana wake. Alisema, walifika na kuzungumza nae, na sasa kijana wake amerejea masomoni skuli ya Mbuzini kwa ajili ya...