Posts

Showing posts from August, 2022

CHAPO: WANANCHI CHAKE CHAKE ENDELEENI KUSHIRIKI ZOEZI LA SENSA

Image
  NA HAJI NASSOR, PEMBA JUMUIYA ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chakechake 'CHAPO' imewakumbusha wananchi wilayani humo, kuendelea kushirikiana na makarani wa sensa, ili kufanikisha zoezi hilo. Wito huo umetolewa leo August 25, mwaka 2022 na Mkurugenzi wa 'CHAPO' Nassor Bilali Ali wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi, juu kuelekea zoezi linaloendelea la sensa ya watu na makaazi.  Alisema ni vyema kwa wananchi kuhakikisha wanaandaa na kupanga shughuli zao vizuri, ili makarani wa sensa watakopfika kutaka taarifa iwe rahisi kupatikana. Mkurugenzi huyo alisema zoezi hilo huja kila baada ya miaka 10, hivyo ni wajibu kwa wananchi kufurahia na kushiriki vyema, ili serikali iweke mipango na mikakati yake vyema vya maendeleo. "Wananchi wa wilaya ya Chakechake tunawaomba kuwa tayari zoezi hilo la sensa limeshaanza tokea August 23, mwaka huu, hivyo ni wajibu kwao kushirikiana na masensa pale watakapofika kwenye maeneo yao kwa kuhesabiwa,"alisema. Katika hatua ...

WANANCHI DODO PEMBA WAIPA TANO CHAPO

Image
  NA HAJI NASSOR, PEMBA WANANCHI wa shehia ya Dodo wilaya ya Mkoani Pemba, wameipongeza Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake ‘CHAPO’ kwa uamuzi wake wa kuwafuata na kuwape elimu ya umuhimu wa upimaji wa ardhi zao, ambao unaweza kuwa suluhu ya migogoro. Walisema zipo tasisi kadhaa, zimaekuwa zikijifungia ndani na kukaa na wataalamu wao ofisini, huku wananchi wakikosa uwelewa wa mambo kadhaa, ingawa kwa ‘CHAPO’ wao hilo hawakulibali. Wakizungumza kwenye mkutano wa wazi, ulioandaliwa na ‘CHAPO’ kwa kushirikiana na ‘the foundation for civil Society na Search for Common Ground’ na kufanyika August 4, 2022 skuli ya Dodo, walisema uamuzi huo, unafaa kuungwa mkono. Wananachi hao walisema, elimu ya njia ya utatuzi wa migogoro kwa njia ya amani, umuhimu wa kusajili ardhi, utambuzi wa mipaka na kuitumia Kamisheni ya wakfu kwenye urithi, ni mambo mema kwao. Mmoja kati ya wananchi hao, Faki Shaib, alisema CHAPO imefanya jambo jema, na wameona umuhimu wa kuhudhuria mku...