MDHAMINI KATIBA, SHERIA: 'AWAPA TANO WASAIDIZI WA SHERIA PEMBA'
NA HAJI NASSOR, PEMBA:: AFISA Mdhamini wizara ya nchi afisi ya rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Pemba Halima Khamis Ali, amesema kazi inayofanywa na wasaidizi wa sheria na watoa msaada wa kisheria, imesaidia kuonesha jamii njia ya haki na kuacha batili. Afisa Mdhamini huyo aliyaeleza hayo, ukumbi wa wizara hiyo, kwenye mkutano wa robo mwaka, wa masuala ya msaada wa kisheria, ulioandaliwa na Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria Zanzibar. Alisema, licha ya changamoto kadhaa walizonazo watoa na wasaidizi hao wa msaada wa kisheria hao, lakini kwa sasa hali inaridhisha ya wananchi, kuzijua haki zao mbali mbali. Alieleza kuwa, jamii awali haikuwa na uwelewa mpana wa haki zao mbali mbali, lakini baada ya Idara ya Katiba na Msaada wa sheria kuwajengea uwezo na kisha kwenda mtaani, hali inaridhisha. ‘’Kwa haki bado msingi mkuu kwa jamii kuzipata na kuzijua haki zao zitabakia kuwa, zimeimarisha na watoa na wasaidizi wa sheria waliomo shehiani, kwa hili hongere ni,’...