Posts

Showing posts from October, 2023

CHAPO YAWAONESHA NJIA WANA WAWI KUEPUKA MIGOGORO YA ARDHI

Image
    NA ASHA ABDALLA, PEMBA WANANCHI wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake, wametakiwa kutafuta hatimiliki kutoka serekalini, maratu baada ya kununua kiwanja,   shamba au kipande cha aina yoyote cha ardhi, ili kuepukana na migogoro isiyokuwa ya lazima.   Hayo yameelezwa Oktoba 28, 2023 na Mjumbe wa Bodi kutoka Jumuiya ya Wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba, ‘CHAPO’ Asha Sleiman Said, wakati akizungumza na wananchi hao, kwenye mkutano wa wazi ulioandaliwa na jumuiya hiyo na kufanyika Kunguni Wawi.   Alisema kua, zipo njia mbali mbali zinazotumiwa ili mtu aweze kupata haki ya kutumia ardhi bila ya migogoro yoyote, ikiwemo njia yakununua na kupewa hati ya matumizi.   Alieleza kuwa, migogoro mingi ya ardhi husababishwa na watu kukosa hati za matumizi pamoja na kuwekeana mipaka inayoondoka kama vile miti na mifimbi ya mito na maziwa.   Mjumbe huyo kutoma CHAPO, alifahamisha kuwa, mwarubaini pekee mara baada ya mtu k...

‘TCACL’: ELIMU IWE NYUNDO YA KUVUNJIA VIKWAZO VYA MTOTO WA KIKE’

Image
  NA HAJI NASSOR, PEMBA MKUU wa Program za Mtandao wa Kupinga Utumikishwaji wa Watoto Tanzania ‘TCACL’ Adam Matiko Charles, amesema wakati Afrika, ikiadhimisha siku ya haki za binaadamu, lazima jamii iondokane na mawazo pekee kuwa, elimu ni haki ya msingi, na waifanye kuwa nyundo ya kuvunja vikwazo kwa mtoto wa kike. Alisema, jamii bado inamtazamo wa zamani juu ya elimu, kama haki ya kawaida ya msingi kwa mtoto, lakini wakati umefika sasa, kuifanya nyundo yenye kuvunja na kupasua vikwazo, vinavyomzungumka mtoto wa kike. Mkuu huyo wa Program, aliyasema hayo skuli ya msingi ya Dk. Philipi Mpango, Gombani Chake chake kisiwani Pemba, wakati akizungumza na wanafunzi, waalimu, wazazi na watetezi wa haki za binaadamu, kwenye maadhimisho ya siku ya haki za binaadamu Afrika. Alisema, siku hiyo ni muhimu kwa jamii, kuangalia ikiwa kuna vikwazo mbali mbali kwa mtoto wa kike, na kuangalia uwezekano kwa kuviondosha kupitia elimu wanayoipata. ‘’Kwa sasa, lazima elimu bora na yenye ma...

CHAPO YAACHA UJUMBE KWA WANAOWAFUNGIA NDANI WATU WENYE ULEMAVU

Image
    NA MWANDISHI MAALUM, CHAPO@@@@ JUMUIYA ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba CHAPO, imewataka wananchi wa kijiji cha Tondooni, shehia ya Wesha wilayani humo, kujua kuwa, kumfungia ndani mtu mwenye ulemavu, ni kosa kisheria kwa vile kumkosesha haki zake za binaadamu. Wito huo umetolewa na Msaidizi wa sheria jimbo la Wawi Haji Nassor Mohamed, wakati, akiwasilisha mada ya haki za binaadamu, kwa wananchi wenye ulemavu, kwenye mkutano wa wazi, ulioandaliwa na ‘CHAPO’ na kuendeshwa na wasaidizi wa sheria. Alisema, hakuna sababu ya mzazi, mlezi kumfungia ndani mtoto mwenye ulemavu, kwa sababu ya ulemavu wake, hivyo kisheria anatakiwa kupelekwa kwenye vituo vya elimu, bila ya kujali aina ya ulemavu aliyonao. Alisema, serikali kwa upande wake imeshaweka mazingira rafiki kiasi, kwa wanafunzi wenye ulemavu na mahitaji maalum, ikiwemo kuanzisha madarasa mjumuishi, kuweka vitengo pamoja na kuanzisha sheria ya kuwalinda. ‘’Kwa mfano ipo sheria mpya ya watu wen...