BARAZA LA WATOTO WESHA, LAWATUNISHIA MISULI WASHUGHULIKIAJI KESI ZA UDHALILISHAJI
NA MWANDISHI MAALUM, CHAPO@@@@ BARAZA la watoto wa shehia ya Wesha wilaya ya Chake chake Pemba, wamesema vitendo vya ukatili na udhalilishaji vitaendelea kuwepo na kuwaathiri, kwa vile watendaji, washughulikiaji, watoaji hukumu, wapelelezi na madaktari ni watu wazima na sio katika kundi lao. Walisema, wapo watoto wenzao wamedhalilishwa na wengine kupata ulemavu wa kudumu na hata kusababisha vifo, ingawa kesi hizo, zinapopelelezwa na kufikishwa mahakamani, watuhumiwa huachiwa huru. Hayo wameyasema Disemba 17, 2023 kwenye mkutano wa wazi ulioandaliwa na Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’ na kufanyika uwanja wa mikutano nyumbani kwa sheha wa shehia ya Wesha, wilayani humo. Wamesema, inashangaaza kuona kesi zinazowahusu watoto kudhalilishwa au kufanyiwa ukatili, zinapelelezwa na kutolewa ushahidi, ingawa kisha hufutwa na kuwaacha wao na maumivu. Katibu wa Baraza hilo Zainab Kassim Juma, alisema kwa vile watoto ndio wanaodhalilishwa na ...