Posts

Showing posts from March, 2023

MSAIDIZI WA SHERIA WAWI, AKAGUZWA ARDHI INAYODAIWA KUVAMIWA NA SERIKALI

Image
  NA MWANDISHI WETU, CHAPO@@@@ MKURUGENZI wa Jumuiya ya Wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Nassor Bilali Ali, amewataka wamiliki wa ardhi wanaoishi mbali nazo, kujenga utamaduni wa kuzikagua kila, wakati, ili kuepushwa kuvamiwa . Mkurugenzi huyo aliyasema hayo Machi 24, 2023, eneo Kwasharifuali shehia ya Wawi, wakati akizungumza na walalamikaji wa eneo hilo, walilodai kuvamiwa na Kiwanda cha mafuta ya makonyo zaidi ya miaka sita sasa, kwa shughuli za upandaji wa miti ya biashara. Alisema, ardhi iliyokaa bila ya kuendelezwa na kisha mmiliki kushindwa kuipitia kila wakati, huwa rahisi mtu yeyote kuanzisha matumizi. Alieleza kuwa, kama mmiliki anaishi mbali na ardhi husika, ni vyema wakaanzisha uwakala wa ulinzi wa ardhi zao, ili iwe rahisi kupatikana taarifa kwa aina yoyote ile ya matumizi. Mkurugenzi huyo wa CHAPO alisema, wamekuwa wakijitahidi kutoa elimu kwa wananchi mbali mbali, juu ya umuhimu wa matumizi ya ardhi. ‘’Wananachi tunawashauri kama wana ardhi ambaz...

..........FUATILIENI MABADILIKO YA SHERIA MSIJEWAPOTOSHA WANANCHI

Image
  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WASAIDIZI wa sheria nchini, wameshauriwa kuwa wafuatiliaji na kujisomea zaidi, ili kujua mabadiliko ya sheria, ili kuwarahisishia wanapokwenda kwa wananchi kutoa elimu. Ushauri huo umetolewa Machi 30, 2023 na Afisa wa Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria Zanzibar Ali Haji Hassan, wakati akiwasilisha mabadiliko ya sheria, ikiwemo ya Ushahidi nambari 9 ya mwaka 2016, kwenye mafunzo kwa njia ya zoom kwa wasaidizi wa sheria. Alisema, moja ya jukumu la msaidizi wa sheria ni kufuatilia kwenye mamla husika, ili kujua ikiwa kuna mabadiliko ya aina yoyote, ili yamsaidie katika utoaji wake wa elimu kwa jamii. ‘’Sisi wasaidizi wa sheria na wengine, tuweni makini kila wakati ili kutambua ikiwa kuna mabadiliko ya sheria au matamko mengine, ili tuwalishe wananchi chakula halali,’’alisisitiza. Akizungumzia mabadiliko ya sheria ya ushahidi iliyokuwa ya mwaka 1917 na kupatikana kwa sheria nambari 9 ya mwaka 2016, alisema imekuja kuweka mazingira mazuri kwa mas...

KAMPENI YA RAIS SAMIA YA 'MSAADA WA KISHERIA' YATAMBULISHW KWA WADAU PEMBA

Image
  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ AFISA Mdhamini wizara ya nchi, afisi ya rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa Utawala bora Pemba, Halima Khamis Ali, amesema kampeni ya kitaifa ya Rais ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mama Samia Suluhu Hassan ya msaada wa kisheria, inalenga kutoa ulinzi na upatikanaji haki, kwa wanawake, watoto na wale wa makundi maalum. Afisa Mdhamini huyo aliyasema hayo Machi 28, 2023, ukumbi wa wizara hiyo Gombani Chake chake Pemba, kwenye mkutano maalum wa kuutambulisha mkakati wa kampeni hiyo, kwa wadau wa haki jinai wakiwemo wasaidizi wa sheria kisiwani humo. Alisema, kampeni hiyo iliyopewa jina la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kutokana na maono yake ya kwa makundi hayo na mengine, ya upatikanaji wa msaada wa kisheria, kampeni hiyo inakuja kuondoa changamoto hizo. Alieleza kuwa, kampeni hiyo inagusa kila taasisi katika utekelezaji wake, ikiwemo wasaidizi wa sheria, Jeshi la Polisi, Tume ya haki za bindamu, vyombo vya sheria, Ofisi za ustawi, wizara husika...

MDHAMINI KATIBA, SHERIA PEMBA AZIITA JUMUIYA NYINGINE KUIGA KWA 'CHAPO'

Image
    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ AFISA Mdhamini wizara ya Nchi, Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Pemba, Halima Khamis Ali, amesema mpango wa kuandaa, darasa la soma la sheria ngazi ya jamii, uliobuniwa na Jumuia ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’ unafaa kuigwa na Jumuiya nyingine. Afisa Mdhamini huyo, aliyesema hayo ukumbi wa Kiwanda cha Makonyo Wawi wilayani humo, wakati akiyafungua mafunzo ya siku 10, kisheria kwa wananchi 20 wa shehia ya Wawi. Alisema, CHAPO imeanzisha mpango mzuri, ambao utasiaidia kwa kiasi kikubwa, ile kiu ya serikali kuu, ya kutaka wananchi wawe na uwelewa wa masuala ya kisheria. Alieleza kuwa, pamoja na kwamba Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria ipo kwa kazi, hiyo lakini ni jambo la faraja kwa Jumuiya ya ‘CHAPO’ kutanua wigo wa elimu ya kisheria. ‘’Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria kwa kushirikiana kwa karibu na skuli ya sheria Zanzibar, imekuwa ikizalisha wasiaidizi wa sheria, lakini kisha ...

CHAPO KUZINDUA MAFUNZO MAALUM YA KISHERIA WAWI MACHI 11, 2023

Image
    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ JUMUIYA ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’, asubuhi ya leo, inatarajia kufungua mafunzo maalum ya sheria ngazi ya jamii, kwa lengo la kuwapa uwelewa wanajamii. Akizungumza na mwandishi wa habari wa hizi ofisini kwake leo Machi 10, 2023 mjini Chake chake, Mkurugenzi wa ‘CHAPO’ Nassor Bilali Ali, alisema, tayari kila kitu kimeshakamilika kuelekea mafunzo hayo. Alisema, mafunzo hayo ya kwanza na maalum kufanywa kwa aina yake, ni miongoni mwa mpango kazi wa ‘CHAPO’ katika kuwaelimisha wananchi masuala ya kisheria. Alieleza kuwa, ‘CHAPO’ inaamini kila mwananchi anayo haki ya kupata uwelewa wa masuala ya kisheria, na ndio maana ‘CHAPO’ ikabuni mpango huo. Mkurugenzi huyo alifafanua kuwa, mafunzo hayo kwa kuanzia, yataanzia shehia ya Wawi kama eneo la majaribio, na kisha kusambaa katika majimbo manne ya wilaya ya Chake chake. ‘’Uzinduzi wa mafunzo haya yanatarajiwa kufanyika Machi 11, ukumbi wa Kiwanda cha Mafuta ya ...

WANAFUNZI 300 WAFIKIWA NA ELIMU YA HEIDH SALAMA PEMBA

Image
  AMINA AHMED, PEMBA. JUMLA  ya wanafunzi wakike  300  wa Skuli za Sekondari Msuka na Chambani Kisiwani Pemba  wamepatiwa  Elimu juu ya  mafunzo ya Hedhi Salama, Ukatili wa kijinsia, pamoja na haki ya Hedhi salama  kwa Mwanafunzi wa Kike.   Wanafunzi 233 kati ya hao wamepatiwa  taulo za Kike  zenye uwezo wa kudumu miaka miwili  kutoka   ikiwa ni  shamra shamra za kuadhimisha siku ya Wanawake Duniani inayoadhimishwa kila ifikapo  tarehe 8  Mwezi wa 3 Duniani kote.    Msaada wa  taulo hizo kwa Wanafunzi hao uliotolewa na Shirika lisilo la Kiserikali la Smile for Community   ni katika utekelezaji wa Mradi wake wa Run for Binti Marathon, ambao umefadhiliwa na Shirika la Msaada  wa Kisheria Legal Services Facility unaotekelezwa kwa  LSF na kufanya kazi kwa kushirikana na   Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia wizara ya  Maendeleo ya Jamii Jinsi...