MKURUGENZI 'CHAPO' AONA MBALI KWA WASAIDIZI WA SHERIA
NA HAJI NASSOR, PEMBA MKURUGENZI wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’ Nassor Bilali Ali, amesema wakati umefika sasa, kwa sheria ya Msaada wa kisheria Zanzibar, kuweka kipengele cha kuwaruhusu wasaidizi wa sheria, kuingia mahakamani kuwawakilisha wateja wao. Alisema, kwa elimu yao inafaa sana sheria iwaruhusu kuingia mahakama za mwanzo na wilaya, ili wanapokuwa na kesi za mwananchi, na ikifikia wakati wa kwenda mahakamani, sheria iwaruhusu. Mkurugenzi huyo aliyasema hayo Disemba 19, 2022, kwenye mkutano kwa njia ya zoom wa kuwasilisha utafiti wa awali, wa haki ya mwanamke kumiliki mali, uliofanywa Tanzania bara na Zanzibar, kupitia tasisi ya LSF. Alisema, wakati mwengine wasaidizi wa sheria wamekuwa wakiianza na kuendeleza vyema kesi husika, lakini hukorogeka na mwananchi kukosa haki yake, kwa kule kushindwa kujieleza mahakamani. Alieleza kuwa, wakati mwengine sio kila lalamiko mfano la ardhi, huduma, ...