Posts

Showing posts from January, 2025

WASAIDIZI WA SHERIA, WAWI ZIWANI WACHANJA MBUGA

Image
  NA MWANDISHI WETU, PEMBA@@@@ JITIHADA za pamoja na endelevu zinahitajika, ili kuwajenga watoto katika mazingira ya malezi bora katika jamii, kwa lengo la kujinasua na majanga yanayowazunguruka.   Hayo yameelezwa hivi karibuni na Msaidizi wa Sheria kutoka shehiya ya Wawi Haji Nassor Mohamed, alipokuwa akiwasilisha mada juu ya haki za watoto na wajibu wao, kwa wanafunzi wa A lmadrassatul- Muuminina  Syyidat Aishaa , iliyopo Fletini shehia ya Wara wilaya ya Chake chake.   Alisema kila mmoja ana haki zake na wajibu wake katika maisha  ya kila siku hivyo kukiwa na malezi ya pamoja, jamii itakuwa na mazingira bora ya kuishi kwa watoto wa leo na kesho.   ”Haki zenu watoto moja wapo ni kupatiwa elimu kama hii ya Madrassa,skuli, pia kupewa majina mazuri, kupatiwa huduma nyengine mbali mbali ambazo haziharibu taratibu za mila na desturi,"alisema.   Katika hatua nyingine, Msaidizi huyo wa sheria shehia ya Wawi, Haji Nassor Mohamed, aliwataka wanafunzi hao kufua...

PICHA ZA MKUTANO WA BODI YA CHAPO NA WANACHAMA WAO

Image
  MKURUGENZI wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba, CHAPO Mohamed Hassan Abdallah, akizungumza na wajumbe wa Bodi ya wadhamini wa CHAPO na wanachama wao, katika mkutano wa dharura uliofanyika ofisini hapo Januari 25, 2025. WA Kwanza kushoto ni Mjumbe wa Bodi ya wadhamini wa CHAPO Zuwena Hamad Ali, akimsikiliza Mkurugenzi wa CHAPO kwenye kikao hicho MWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini wa CHAPO Safia Saleh Sultan, akimsikiliza Mwanachama wa CHAPO Wahida Kombo Khamis, kwenye kikao hicho.

JAMII YATAKIWA KUWAUNGA MKONO WASAIDIZI WA SHERIA MAPAMBANO YA UDHALILISHAJI

Image
    NA MWANDISHI WETU, PEMBA@@@@ JAMII imetakiwa kuunga mkono juhudi zinazofanywa na wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba, katika kupiga vita vitendo vya mbali mbali vya kihalifu vikikiwemo vile vya ukatili na udhalilishaji.   Wakitoa elimu juu ya kuviepuka vitendo hivyo kwa wanafunzi Januari 23, 2025 wa Madrassatul Nuru-lhuda ya kijiji cha Tondooni shehiya ya Wesha, wasaidizi hao wa sheria walisema watendaji wa vitendo hivyo hufanyaji siri, na ndio maana nguvu za pamoja na zinahitajika.   W alisema, kama juhudi zinazofanywa na wasaidizi wa sheria zitaungwa mkono na jamii, kunauwezekano mkubwa kwa kiasi falani matendo hayo kupungua, kwani watendaji wanaishi kwenye jamii. Akitoa mada juu ya udhalilishaji msaidizi wa sheria kutoka shehiya ya Mgogoni wilayani humo, Jaffar Abdalla Ali, alisema watendaji hutumia mbinu mbali mbali, kabla ya kuwadhilishaji watoto ikiwemo kuwapa zawadi.   Alieleza kuwa, ni vyema watoto kwa sasa wakawa na utamaduni wa kutoa t...

CHAPO: YAKABIDHI MSAIDIZI WA SHERIA SHEHIA YA MGOGONI

Image
    NA MWANDISHI MAALUM, PEMBA@@@@ WASAIDIZI wa sheria kutoka Jumuia ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba, ‘CHAPO’ wametakiwa kufanya kazi kwa ushirikiano mkubwa na jamiii, ilikuondosha migogoro kwa njia ya kuiripoti katika sehemu zinazohusika kisheria. Hayo yameelezwa Januari 21, 2025  na wajumbe wa kamati wa sheha wa Mgogoni wilayani humo, mara baada ya kumtambulisha Msaidizi wa sheria Jaffar Abdalla Ali, anayetarajiwa kufanyakazi katika shehia hiyo, hafka iliyofanyika kijiji cha Mgogoni.   Walisema kuwa katika shehia hiyo, kumekuwa na matukio mengi ambayo hayana mshughulikiaji wa moja kwa moja kisheria, hali inayopeleka watu wengi kukosa haki zao kutokana na kukosa eneo husika la kuzidai.   Akimtambulisha msaidizi huyo wa sheri, kiongozi wa timu ya wasaidizi wa sheria, kutoka Jimbo la Wawi Haji Nassor Mohamed, aliwaambia wajumbe hao kuwa, kufanyakazi kwa karibu na Msaidizi huyo wa sheria.  Alisema, kwa muda mrefu shehia hiyo ilikosa Msaidiz...

CHAPO: ‘WASAIDIZI WA SHERIA ONGEZENI BIDII KUWAFIKIA WANANCHI’

Image
NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WASAIDIZI wa sheria wilaya ya Chake chake, wamekumbushwa kuongeza bidii ya kufikia jamii, ili kuwapa elimu, msaada na ushauri wa kisheria bila ya malipo, kwa vile ndio ahadi ya kazi yao hiyo. Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilayani humo Mohamed Hassan Abdalla, wakati akizungumza na watendaji hao, kwenye kikao cha mwezi cha kawaida, kilichofanyika ofisini kwao mjini Chake chake. Alisema, kila msadizi wa sheria anaelewa wajibu huo, hivyo ni vyema kuendelea kuifanyia kazi kwa bidii, kwani wananchi waliokata tamaa ya kupata hazi za kisheria, wanawategemea wao, kutokana na kukosa uwezo wa kuwafikia wanasheria. Alieleza kuwa, wajibu huo wakiuupuza na kuusahau wajue fika kuwa, wanawakosesha haki wananchi wingine hasa wale wenye kipato cha chini, ambao kwa kiasi kikubwa wananategemea wao. Mkurugenzi huyo alifahamisha kuwa, ijapokuwa kazi kubwa kwa mwaka 2024 ilifanywa na wasaidizi wa sheria hao, lakini ni vyema wakaongeza juhudi ya kaz...