Posts

SHEHIA YA MVUMONI WAZINDUA KAMATI YA KUPINGA UDHALILISHAJI

Image
  NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ MKUU wa Idara ya Wazee na Ustawi wa Jamii Pemba, Omar Mohamed Ali amesema kuwa kuundwa kwa kamati ya kupinga na kupambana na vitendo vya udhalilishaji, itasaidia kwa kiasi kikubwa, kuandaa jamii yenye ustawi bora ambayo itawaweka wanawake na watoto, katika mazingira yaliyosalama. Alisema kuwa vitendo vya ukatili na udhalilishaji kwa wanawake na watoto, bado vinaendelela kujitokeza katika jami, hivyo serikali, inaendelea kutumia mbinu tofauti, ikiwemo kuunda kamati za shehia, wilaya, mkoa na taifa, ili kupambana na na vitendo hivyo. Aliyasema hayo katika uzinduzi wa kamati ya kupinga udhalilishaji dhidi ya wanawake na watoto shehia ya Mvumoni, hafla iliyofanyika skuli ya sekondari ya Furaha. Alieleza kuwa, kuwepo kwa vitendo hivyo vimekuwa vikiwarudisha nyuma, baadhi ya jamii kwa kuona muhali wa kuviripoti, hivyo uwepo wa kamati hiyo inaweza kuwa mwarubaini.   "Nendeni mkafanye kazi kwa kuielimisha jamii, juu ya athari ya vitendo vya ukatili ...

WAZO LA MSAIDIZI WA SHERIA LAKUBALIWA MVUMONI

Image
  NA AISHA MOHAMED, PEMBA@@@@ MSAIDIZI wa sheria shehia ya Mvumoni wilaya ya Chake Chake Pembaa, Haji Nassor Mohamed, ameutaka uongozi wa shehia hiyo, kuifufua kamati ya kupambana na vitendo vya udhalilishaji, ili vitendo hivyo visiendelee kuwathiri wanawake na watoto.   Msaidizi huyo wa sheria, aliyasema hayo jana kituo cha afya Mvumoni, kwenye mkutano maalum unaolenga, kuifufua kamati hiyo, na kuhudhuriwa na wajumbe wa sheha na mratibu wa wanawake na watoto wa shehia hiyo.   Alisema   lengo la kikao hicho ni kuja kuifufua kamati ya kupambana na vitendo vya udhalilishaji, ambayo ilionekana kusizi, ili kuweza kuvipunguza vitendo hivyo shehiani humo.   Alisema vitendo vya udhalilishaji vipo katika shehia za wilaya ya Chake chake ikiwemo ya Mvumoni, hivyo ni wakati sasa kuifufua na wajumbe wake wake, kufanyakazi wa bidi.   “Nawaomba sana wajumbe wa kamati na sheha mwenyewe, tushirikiane na mratibu wetu wa wanawake na watoto wa shehia, ili ku...

CHAPO: ‘WAZAZI CHAKE CHAKE MSIWARUHUSU WATOTO KUOMBA 'MKONO WA IDD’

Image
    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ JUMUIYA ya wasaidizi wa sheria, wilaya ya Chake chake ‘CHAPO’, imewataka wazazi na walezi wilayani humo, kuwakataza watoto, kuacha utamaduni wa kuomba fedha za sikukuu ‘ mkono wa idd’ katika maeneo ya mbali na wanapoishi. Kauli hiyo imetolewa leo Mei 26, 2026 na Mkurugenzi wa Jumuiya hiyo jana, Mohamed Hassan Abdalla, wakati akitoa taarifa kwa waandishi wa habari, kuelekea sherehe ya sikukuu ya kiislamu. Alisema, utamaduni wazazi kuwaruhusu watoto wao kuomba fedha kipindi cha sikukuu, huwa ni chanzo kikuu cha udhalilishaji ambao unaepukika. Alieleza kuwa CHAPO, inawapenda mno watoto wa wilaya hiyo, na ndio maana, inaendelea kuwasisitiza wazazi na walezi wao, kuondokana na mpango huo. Mkurugenzi huyo alifafanua kuwa, kwani wapo baadhi ya vijana na hata watu wazima, wanaweza kuchukua fursa hiyo ya kuwadhalilisha watoto hao. ‘’Wapo baadhi ya watoto wanatoka kijiji kimoja hadi chingine, kisa ni siku ya sikukuu, hugonga kila nyumba kuomba fedha ‘ mkon...

MRAJISI WA NGOs: ‘ZAPONET’ JIPANGENI KUJITEGEMEA WENYEWE

Image
    NA HAJI NASSOR, UNGUJA@@@@ MRAJISI wa asasi za kiraia Zanzibar Ahmed Khalid Abdulla, amesema mtandao wa wasaidizi wa sheria Zanzibar ‘ZAPONET’ ianze sasa kujipanga vyema kuhakikisha wanajiendesha wenyewe, na sio kutegemea wafadhili. Mrajisi huyo aliyasema hayo leo Januari 25, 2026 ukumbi wa Malaria Mwanakwerekwe Unguja, wakati akiufungua mkutano mkuu wa kwanza wa mwaka ‘ZAPONET’, uliokuwa na malengo kadhaa, ikiwemo mapatio ya katiba na uwasilishaji wa ripoti za wanachama wao. Alisema, ZAPONET ni muhimili muhimu kwa jumuia za wasaidizi wa sheria, lakini kikubwa kwa sasa ni kujipanga mapema, ili kujiendesha yenyewe na kutoa usaidizi kwa wanachama wao. Alieleza kuwa, msingi wa wasaidizi wa sheria kutoa elimu, ushauri na msaada wa kisheria kwa jamii bila ya malipo, inazingalia sana jumuia zao pamoja na mtandao huo, katika kuwajengea uwezo. Alifafanua kuwa, ingawa kwa sasa wanaendelea kushikwa mkono na taasisi ya LSF, na kufanya vizuri katika utendaji wao wa kazi. ‘’...

WAJUMBE SHEHIA MVUMONI WAPIGWA MSASA ELIMU YA KISHERIA

Image
    NA MWANDISHI WETU, PEMBA   WAJUMBE wa sheha wa shehia ya Mvumoni wilaya ya Chake chake, wameelezwa kuwa, suala la haki za binaadamu sio la kuomba, bali ni haki ya kila mmoja, kwa ubinaadamu wake.   Mkurugenzi wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilayani humo ‘CHAPO’ Mohamed Hassan Abdall, aliyasema hayo leo Disemba 7, 2025 wakati akiwasilisha mada ya haki za binaadamu, kwa wajumbe hao, kwenye mafunzo ya siku moja.   Alisema, haki za binaadamu, ni haki zote anazostahiki mtu, kwa sababu ya kuwepo kwake duniani, ikiwemo uhai, matibabu, afya, elimu, utaifa na uzalendo.   ‘’Niwaombe sana wajumbe wetu wa shehia ya Mvumoni, kwanza elimu hii mkawafikishie na wingine, maana haki za binaadamu ni zote,’’alieleza.   Akizungumzia faida za kufanya sulhu kwa kesi za madai kama vile, huduma za mke, watoto, migogoro ya ardhi, mirathi na madeni, alisema inaondosha visasi. Alifahamisha, kuwa ndio maana, wamempeleka msaidizi wa sheria katika eneo lao...