Posts

CHAPO: ‘WAZAZI CHAKE CHAKE MSIWARUHUSU WATOTO KUOMBA 'MKONO WA IDD’

Image
    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ JUMUIYA ya wasaidizi wa sheria, wilaya ya Chake chake ‘CHAPO’, imewataka wazazi na walezi wilayani humo, kuwakataza watoto, kuacha utamaduni wa kuomba fedha za sikukuu ‘ mkono wa idd’ katika maeneo ya mbali na wanapoishi. Kauli hiyo imetolewa leo Mei 26, 2026 na Mkurugenzi wa Jumuiya hiyo jana, Mohamed Hassan Abdalla, wakati akitoa taarifa kwa waandishi wa habari, kuelekea sherehe ya sikukuu ya kiislamu. Alisema, utamaduni wazazi kuwaruhusu watoto wao kuomba fedha kipindi cha sikukuu, huwa ni chanzo kikuu cha udhalilishaji ambao unaepukika. Alieleza kuwa CHAPO, inawapenda mno watoto wa wilaya hiyo, na ndio maana, inaendelea kuwasisitiza wazazi na walezi wao, kuondokana na mpango huo. Mkurugenzi huyo alifafanua kuwa, kwani wapo baadhi ya vijana na hata watu wazima, wanaweza kuchukua fursa hiyo ya kuwadhalilisha watoto hao. ‘’Wapo baadhi ya watoto wanatoka kijiji kimoja hadi chingine, kisa ni siku ya sikukuu, hugonga kila nyumba kuomba fedha ‘ mkon...

MRAJISI WA NGOs: ‘ZAPONET’ JIPANGENI KUJITEGEMEA WENYEWE

Image
    NA HAJI NASSOR, UNGUJA@@@@ MRAJISI wa asasi za kiraia Zanzibar Ahmed Khalid Abdulla, amesema mtandao wa wasaidizi wa sheria Zanzibar ‘ZAPONET’ ianze sasa kujipanga vyema kuhakikisha wanajiendesha wenyewe, na sio kutegemea wafadhili. Mrajisi huyo aliyasema hayo leo Januari 25, 2026 ukumbi wa Malaria Mwanakwerekwe Unguja, wakati akiufungua mkutano mkuu wa kwanza wa mwaka ‘ZAPONET’, uliokuwa na malengo kadhaa, ikiwemo mapatio ya katiba na uwasilishaji wa ripoti za wanachama wao. Alisema, ZAPONET ni muhimili muhimu kwa jumuia za wasaidizi wa sheria, lakini kikubwa kwa sasa ni kujipanga mapema, ili kujiendesha yenyewe na kutoa usaidizi kwa wanachama wao. Alieleza kuwa, msingi wa wasaidizi wa sheria kutoa elimu, ushauri na msaada wa kisheria kwa jamii bila ya malipo, inazingalia sana jumuia zao pamoja na mtandao huo, katika kuwajengea uwezo. Alifafanua kuwa, ingawa kwa sasa wanaendelea kushikwa mkono na taasisi ya LSF, na kufanya vizuri katika utendaji wao wa kazi. ‘’...

WAJUMBE SHEHIA MVUMONI WAPIGWA MSASA ELIMU YA KISHERIA

Image
    NA MWANDISHI WETU, PEMBA   WAJUMBE wa sheha wa shehia ya Mvumoni wilaya ya Chake chake, wameelezwa kuwa, suala la haki za binaadamu sio la kuomba, bali ni haki ya kila mmoja, kwa ubinaadamu wake.   Mkurugenzi wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilayani humo ‘CHAPO’ Mohamed Hassan Abdall, aliyasema hayo leo Disemba 7, 2025 wakati akiwasilisha mada ya haki za binaadamu, kwa wajumbe hao, kwenye mafunzo ya siku moja.   Alisema, haki za binaadamu, ni haki zote anazostahiki mtu, kwa sababu ya kuwepo kwake duniani, ikiwemo uhai, matibabu, afya, elimu, utaifa na uzalendo.   ‘’Niwaombe sana wajumbe wetu wa shehia ya Mvumoni, kwanza elimu hii mkawafikishie na wingine, maana haki za binaadamu ni zote,’’alieleza.   Akizungumzia faida za kufanya sulhu kwa kesi za madai kama vile, huduma za mke, watoto, migogoro ya ardhi, mirathi na madeni, alisema inaondosha visasi. Alifahamisha, kuwa ndio maana, wamempeleka msaidizi wa sheria katika eneo lao...

SHEHIA YA MVUMONI YAPATA MSAIDIZI MPYA WA SHERIA

Image
  NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ MSAIDIZI mpya wa sheria shehia ya Mvumoni wilaya ya Chake chake Pemba, Haji Nassor Mohamed, ameuomba uongozi wa shehia hiyo, kumpa kila aina ya uhirikiano, ili kufanikisha majukumu yake.   Ameyasema hayo Novemba 29, 2025 alipokuwa akijitambulisha kwa wajumbe wa sheha, mara baada ya kuhamishiwa shehia hiyo akitokea Wawi, kwa lengo la kutoa elimu, ushauri na msaada wa kisheria bila ya malipo.   Alisema kuwa, kubwa analohitaji ni ushirikiano kuanzia kwa sheha, wajumbe na wananchi wa Mvumoni, ili lengo la kuwahudumia wananchi lifikiwe.   Alieleza kua, ataendelea kuwa tegemeo kwa wananchi wa Mvumoni, kwani anaamini wapo ambao hawana uwelewa mpana, wa masuala ya kisheria.   ‘’Kwanza nishukuru kwa kupokelewa, na ninachotaka kubwa zaidi ni umoja, mshikamano na ushirikiano miongoni mwenu,’’alieleza.   Aidha Msaidizi huyo wa sheria, aliwakumbusha wajumbe hao wa sheha, kutokubali kuzifanyia sulhu kesi za jinai na hasa z...

AFISI YA MWANASHERIA MKUU ZANZIBAR YAKUSANYA MAONI SHERIA YA MSAADA WA KISHERIA

Image
  NA HAJI NASSOR, PEMBA @@@@ AFISA Mdhamini wizara ya Nchi Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Pemba, Halima Ali Khamis, ameitaka Afisi ya Mwanasheria Mkuu Zanzibar ‘AGCZ’ kurudi tena kwa wadau, baada ya kuyachakata maoani ya sheria nambari 13 ya mwaka 2018 ya Msaada wa Kisheria Zanzibar.   Mdhamini huyo aliyasema hayo leo Novemba 13, 2025 , ukumbi wa wizara ya Fedha Pemba, alipokuwa akifungua kikao kazi, cha kukusanya maoni ya sheria ya Msaada wa Kisheria, mbele ya wadau wakiwemo wasaidizi wa sheria, Polisi, Masheha na wadau wa haki za binaadamu. Alisema itapendeza zaidi, baada ya kukusanya maoni hayo kwa Afisi ya Mwanasheria Mkuu kurudi tena kwa wadau, ili kujadiliana kabla ya kuandikwa, kama sheria ya msaada wa kisheria. Alieleza kuwa, wadau wanataka kuona maoni yao, ikiwa yamezingatiwa kwa kiasi gani, kwenye uandikwaji wa sheria hiyo upya hapo baadae. ‘’Niwaombe sana wenzetu wa ofisi ya 'AGCZ', mkumbuke kurudi tena kwa wadau, baada ya kukusanya ...

WAGOMBEA CCM JIMBO LA CHAKE CHAKE, KUANZISHA WIKI YA MSAADA WA KISHERIA

Image
    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MGOMBEA Ubunge na Uwakilishi jimbo la Chake chake, wamesema kama wakipata ridhaa ya wananchi, wataanzisha wiki ya msaada wa kisheria jimboni humo, ili kuwasaidia wananchi, wenye changamoto za kisheria.   Walisema, wanayodhamira ya dhati kuhakikisha wananchi wa jimbo hilo, wanaondokana na changamoto za kisheria, kwa kuanzisha wiki ya msaada wa kisheria, kila baada ya muda.   Wakizungumza na baadhi ya watendaji wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’, wakati walipofika ofisini hapo, walisema wanachosubiri ni ridhaa tu ya wananchi.   Wagombea hao walisema, wamebaini kuwa, ipo haja ya kuongeza nguvu ya kutoa elimu, msaada na ushauri wa kisheria kwa wananchi, na hilo litawezekana kwa kuanzisha wiki ya msaada wa kisheria.   Mgombea Uwakilishi Abdulla-wahabi Said Abubakar, alisema kwa kushirikiana na viongozi wenzake, na baada ya kukaa na uongozi wa ‘CHAPO’, azma hiyo wanayo. ...

BODI CHAPO YANG'AKA UTORO, UVIVU WA WASAIDIZI WA SHERIA

Image
  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WAJUMBE wa Bodi wa Jumuiya ya Wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’, wamesema hawataki kusikia tena kuwa, wapo wasaidizi wa sheria, wamekuwa wavivu wa kufanya wajibu wao na kudharau vikao vinavyoitwishwa. Walisema, kila mmoja anajua kuwa, CHAPO kama ilivyo wa jumuiya nyingine, ni eneo la kujitolea, sasa kama wako tayari kuendelea nayo, wahakikishe wanaendelea kuwahudumia wananchi. Mwenyekiti wa Bodi hiyo Safia Saleh Sultan, alisema wakati wanaomba kuingia kwenye sekta ya wasaidizi wa sheria, suala la kujitolea na kujitoa, ndio kigezo kikuu. Alieleza kuwa, leo anashangaa kusikia kuwepo wasaidizi wa sheria ndani ya ‘CHAPO’, wamekuwa wavivu wa kutoa elimu na msaada wa kisheria kwa jamii. Alifahamisha kuwa, uvivu wao wa kufanyakazi na jamii, inaweza kupoteza mwelekeo kwa wananchi, na kuiangusha CHAPO, jambo ambalo akiwa Mwenyekiti, hataki kulisikia. ‘’Kila mmoja kuanzia sasa afanye wajibu wake, ambao ni kutoa elimu, ushauri na...