Posts

Showing posts from August, 2025

WANACHAPO WAPEWA MAFUNZO AKILI MNEMBA 'AI'

Image
  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANACHAMA wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’ wamepatiwa mafunzo ya matumizi ya akili ya kisayansi ‘akili mnemba’, baada ya watendaji wa wawili wa jumuiya hiyo, kumaliza mafunzo kama hayo, wiki iliyopita. Kabla ya kuanza kwa mafunzo hayo, Mkurugenzi wa ‘CHAPO’ Mohamed Hassan Abdalla, alisema utaratibu kwa sasa utakuwa kwa kila atakayerudi kwenye mafunzo, kuhakikisha anawapa na wenzake. Alisema, mpango huo ulikuwepo zamani, ingawa katika siku za hivi karibuni, ulionekana kufa, na wakati umefika sasa kuufufua, ili kuona nguvu zinazotumiwa na washirika wao, zinaungwa mkono. Akitoa mada ya mafunzo hayo ofisini kwao Chake chake jan August 17, 2025, alisema akili mnemba, ni mfumo wa kompyuta ambao umeshajazwa taarifa kadhaa, ambazo ni za ukweli, kwa ajili ya matumizi. Alisema, utaalaamu baada ya kuendelea, mifumo hiyo hujazwa taarifa rasmi, na kisha kwa kutumia mifumo ya tovuti za ‘GPT’, unaweza kuipakua na kuuliza mas...

‘YALETENI MALALAMIKO YA KUVUNJIWA HAKI ZENU TUME’

Image
    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI wa shehia ya Mjananza wilaya ya Wete Pemba, wameshauriwa kuyafikisha malalamiko yao ya kisheria, yanayohusu uvunjwaji wa haki zao, kwa Tume ya Haki za Binaadamu na Utawala Bora, ili kupata ufafanuzi. Hayo yalieleza leo August 14, 2025 kijiji cha Mlalashi shehiani humo, na Mwanasheria kutoka Tume hiyo Pemba, Mohamed Massoud, wakati akielezea majukumu ya taasisi hiyo, kwenye mkutano wa wazi, ulioandaliwa na Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria Zanzibar. Alisema, moja ya jukumu la tume hiyo, ambayo ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ni kupokea, kusikiliza malalamiko mbali mbali ya uvunjifu wa haki wa binaadamu, tena bila ya malipo. Alieleza kuwa, ofisi yao ambayo kwa sasa ipo Chake chake, inawakaribisha wananchi hao na wingine, ili kufika na kulalamikia, ikiwa wanaona kuna haki yao, iliyovunjwa. ‘’Kwa mfano umevunjiwa nyumba yako, kwa kupisha mradi wa kijamii kama barabara au ujenzi wa skuli na hakuna dalili ya kulipwa fidia, ...

‘WANANCHI HAWANA MAMLAKA YA KUONDOSHA UHAI WA MTU’

Image
  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI wa shehia ya Mchakwe na Mwambe wilaya ya Mkoani, wamekumbushwa kuwa, ni kosa la kisheria, kujichukulia sheria mikononi, kwa kuondoa uhai wa mtu, kwani kufanya hivyo, ni kuzipokonya kazi mamlaka zilizopo kisheria. Hayo yalielezwa jana August 12, 2025 na Wakili wa serikali kutoka ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa serikali Safia Saleh Sultan, wakati akizungumza na wanachi hao, kwenye mkutano wa wazi, ulioandaliwa kwa pamoja na Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria Zanzibar na kufanyika shehiani humo. Alisema, zipo mamlaka ikiwemo mahakama, ndio ambayo inaweza kutoa adhabu ya kifo, ikiwa mshitakiwa atatiwa hatiani. Alieleza kuwa, imezoeleka kuona wananchi wanajichukulia sheria mikononi, mara wanapomkamata mtuhumiwa, jambo ambalo, wajibu wao ni kumfikisha mbele ya vyombo vya sheria. Wakili huyo wa serikali, alisema mahkama pekee ndio ambayo kisheria imepewa nguvu za kisheria, kuondoa uhai wa mtu, ikiwa nae amebainika kuua kwa maksudi. ‘’Imek...

MKURUGENZI HANIFA, AWAUMA SIKIO WANANCHI WAWI HAKI ZA BINAADAMU

Image
      NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MKURUGENZI wa Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar, Hanifa Ramadhan Said, amewataka wananchi wa shehia ya Wawi wilaya ya Chake chake, kulindiana haki zao za binaadamu, ili kujengeana heshima baina yao.   Hayo aliyasema leo August 11, 2025 eneo la Kwa Gerei shehiani humo, wakati akizungumza na wananchi hao, kwenye mkutano wa wazi wa kutoa elimu ya haki za binaadamu.   Alisema kila mmoja anawajibu wa kumlindia haki za binaadamu mwenzake, na kufanya hivyo kutajengeana heshima miongoni mwao.   ‘’Haki za binaadamu ni pamoja na ile ya kuishi na kupata faragha, sasa kama kila mmoja atamlindiana mwenzake, heshima kwa wananchi, itaongezeka,’’alisema.   Hata hivyo Mkurugenzi huyo wa Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria, amewakumbusha wananchi hao, kuwatumia wasaidizi wa sheria, waliomo ndani ya shehia, ili kupata ufafanuzi wa changamoto zao za kisheria.   Mapema Afisa sheria kutoka Ofisi ya M...

IDARA YA KATIBA NA MSAADA WA KISHERIA YAWAALIKA WANANCHI WAWI ELIMU YA KISHERIA LEO HII

Image
    NA HAJI NASSOR, PEMBA WANANCHI wa shehia ya Wawi wilaya ya Chake chake, wametakiwa kuitumia fursa ya kuhudhuria mkutano maalum wa elimu ya kisheria, ulioandaliwa na Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria, unaotarajiwa kufanyika jioni hii ya leo shehiani humo. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Mkuu wa Divisheni ya Idara hiyo Pemba Bakari Omar Ali, alisema mkutano huo, ni maalum kwa ajili ya wananchi hao, ili kuwapa elimu na msaada wa kisheria bila ya malipo. Alisema, mkutano huo ambao utafanyika eneo la Kwa gerei Wawi (Kwa Ali Haji) majira ya saa10:00 jioni, ni sehemu ya utendaji wa kazi wa kawaida wa Idara hiyo, katika kuhakikisha jamii inapata muelekeo wa kutambua haki na wajibu wao kisheria. Alieleza kuwa, zipo njia kadhaa za wananchi kujua haki zao za kisheria, moja wapo ni kuwapelekea wataalam wa sheria ndani ya shehia, na kuelezea changamoto zao za kisheria. ‘’Mkutano huu ambao unatarajiwa kufanyika jioni hii shehia ya Wawi ni maalum, ili kuona wanap...