Posts

Showing posts from November, 2023

WANAKONGAMANO: ‘RUSHWA MUHALI ITAENDELEA KUTUTAFUTA MAPAMBANO DHIDI YA UDHALILISHAJI’

Image
    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WAATHIRIKA wa matendo ya ukatili na udhalilishaji kisiwani Pemba, wamesema pamoja na juhudi za serikali kuweka mazingira ya kupungua matendo hayo ikiwemo kuweka adhabu kali, bado rushwa muhali ni kikwazo katika jamii. Wakizungumza kwenye kongamano la siku moja la kuelekea siku 16 za kupinga ukatili na udhalilishaji, lililoandaliwa na Jumuiya ya Wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba CHAPO, na kufanyika ofisi ya TAMWA Chake chake, washiriki hao walisema bado rushwa muhali ni changamoto. Walisema bado katika jamii, suala la rushwa muhali linaendelea kujitokeza, hali inayosababisha kuimarika kwa matendo ya ukatili na udhalilishaji. Hidaya Mjaka Ali kutoka Umoja wa watu wenye Ulemavu UWZ, alisema, serikali imezirekebisha sheria, kwa kuongeza adhabu ya kuanzia miaka 30 na kuendelea. Alieleza kuwa kama hilo lipo, ni wajibu sasa kwa mahakim na majaji kuzifuata sheria hizo, wakati wa kutoa hukumu, waathirika wapate imani na vyombo vya s...

WANAKONGAMANO: ‘’TUITUMIENI TUME YA KUREKEBISHA SHERIA KUTOA MAONI KWA SHERIA MUITAKAYO’’

Image
  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI kisiwani Pemba, wameshauriwa kuitumia Tume ya Kurekebisha sheria wanapokuwa na vikao vyao vya kupokea maoni, ya kutaka kurekebishwa sheria, ili kuwa na sheria zinazoendana na dunia ya sasa. Ushauri huo umetolewa na wanakongamano la siku moja, la kuelekea siku 16 za kupinga ukatili na udhalilishaji, leo Novemba 28, 2023 lililoandaliwa na Jumuiya ya wasaidizi wa sheria, wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’, na kufanyika ukumbi wa Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba. Walisema, ni vyema wananchi wanapokutana na Tume hiyo, kuacha jazba na kuzitolea maoni sheria, ambazo zimeshapitwa na wakati, ili kueleza wanavyotaka ziwe, kwa mujibu wa mazingira ya sasa. Mjumbe wa Jumuiya ya TUJIPE Pemba, Sheikh Abdalla Nassor Maulid, alisema utoaji wa maoni katika tume hiyo, ni njia muhimu kwa jamii kuwa na sheria rafiki. ‘’Tume ya kurekebisha, hupita katika maeneo yetu, sasa sisi wananchi tuitumieni ili kutoa mao...

WATU WENYE ULEMAVU PEMBA: “BADO HAKI ZETU ZINAPIGWA MATEKE’’

Image
  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WATU wenye ulemavu kisiwani Pemba, wamesema bado wanamashaka na utekelezaji wa haki zao, ikiwemo ajira, miundombinu ya kuyafikia majengo ya umma na upatikanaji huduma za kijamii kwa ina ya mazingira yao. Walisema, wamekuwa na watetezi wengi mno katika taifa, lakini kwenye utekezaji halisi, wanaendelea kukumbana na vikwazo, hali inayosababisha kuwavunja moyo, kwa baadhi ya wakati. Hayo waliyasema Novemba 27, 2023 kwenye kongamano la siku moja, lililoandaliwa na Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’ na kufanyika ofisi ya Umoja wa Watu Wenye Ulemavu ‘UWZ’ Mkanjuni, ikiwa ni muendelezo wa mikutano, ya ndani ya siku 16 za kupinga ukatili na udhalilishaji. Walisema, hadi miaka ya hivi karibuni, yapo majengo ya umma yanajengwa bila ya kuzingatia miundombuni yao, jambo linalowavunja moyo na kujiona wanatengwa. Mjumbe wa ‘UWZ’ Nassor Suleiman, alisema wamekuwa wakijuliza kwamba sasa wafike pahala, wasizungumze jambo lolo...

CHAPO: ‘WAZAZI TENGENI MUDA KUZUNGUMZA NA WATOTO WENU’

Image
  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@   WAZAZI na walezi wa kijiji ch Jamvini shehia ya Ndagoni, wilaya ya Chake chake Pemba, wametakiwa kutenga muda wa kukaa na watoto wao, ili kuwahoji yaliotokezea mchana mzima, kwa lengo kubaini ikiwa wameanza kufanyiwa vitendo vya udhalilishaji ama laa.   Ushauri huo umetolewa Novemba 25, 2023 na Masaidizi wa sheria Jimbo la Ziwani, shehia ya Wesha Khadija Said Khalfan, wakati akizungumza na wazazi na walezi, pamoja na watoto wao, wa kijiji cha Jamvini, ikiwa ni mikutano ya kutoa elimu ndani ya siku 16 za kupinga ukatili na udhalilishaji wa wanawake na watoto.   Alisema, njia moja wapo ya kubaini, iwapo mtoto ameanza kubadili tabia na hasa kwenye vitendo vya udhalilishaji, ni wazazi kutenda muda, wa kukaa na watoto hao.   Alieleza kuwa, hipendezi kuona wazazi hao, wanaelekeza nguvu zao zaidi katika kutafuta maisha pekee, bali waelewa kuwa, sasa ulimwengu umebadilika na yapo majanga ambayo huwakumba watoto.   ...

CHAPO: ‘WAZAZI WALINDENI WATOTO NA MVUA ZINAZONYESHA’

Image
    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ UONGOZI wa Jumuiya ya Wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’ umewakumbusha wazazi na walezi, kuwalinda kwa nguvu watoto, hasa katika kipindi hichi cha mvua, ili kuwaepushia na kukumbwa na ajali kutokana na madimbwi ya maji.   Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Chake Chake, Mkurugenzi wa CHAPO Nassor Bilali Ali, alisema wakati huu mvua zikiendelea kunyesha, ni vyema kwa wazazi na walezi, kuwa makini na watoto wao. Alieleza kuwa, Pemba inayomilima mikubwa iliyotengeneza misingi yenye kupita maji kwa nguvu kuelekea baharini, hivyo ni vyema wazazi wakaongeza ulinzi kwa watoto wao, ili kuepukana na majanga hayo. Mkurugenzi huyo alieleza kuwa, zipo baadhi ya familia kwa kujua ama kutokujua, wameanzisha makaazi maeneo ya mabondeni, ambako maji yanakuwa na nguvu, hivyo kwa kipindi hichi cha mvua za vuli, wakawa makini na jambo hilo. ‘’Sisi CHAPO tunatoa tanbihi ya kuwataka wazazi na walezi, kuhakikisha w...

LFS, YAWAONESHA NJIA MAAFISA MAWASILIANO WA JUMUIYA ZA WASAIDIZI WA SHERIA

Image
  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAAFISA mawasiliano na habari wa Jumuia za wasaidizi wa sheria Tanzania zimetakiwa kujenga ushirikiano wa karibu na watendaji wenzao, ili kuhakikisha wanakuwa na mifumo sahihi ya utoaji wa taarifa za jumuia. Hayo yameelezwa Novemva 24, 2023 na Mtaalamu wa masoko kutoka LSF      Gilsant Mlaseko , wakati akizungumza na maafisa   hao kwenye mkutano wa kujengewa uwezo kwa njia ya kielektroniki. Alisema bidhaa ya mwasiliano sio haki ya Afisa Mawasiliano na Habari pekee kwenye jumuiya, bali anatakiwa kuwa karibu na wakurugenzi, waratibu na watendaji wengine. Alieleza kuwa, wakati mwingine ndani ya Jumuiya Afisa huyo anaweza kuwa mwisho katika utoaji wa taarifa na hasa baada ya kuidhinishwa na kuthibitishwa na kamati iliyoteuliwa. ‘’Suala la mawasiliano hasa ya kutoka nje ya Jumuiya, linapaswa watoa taarifa wawe makini na sio jukumu la mtendaji mmoja, bali iwe ni timu ya Jumuiya na kisha muhusika anateuliwa,’’alieleza. Akiele...

CHAPO: ‘’WANAFUNZI JIEPUSHENI KUFANYIANA UDHALILISHAJI WENYEWE’’

Image
  NA ASHA ABDALLA, PEMBA WANAFUNZI wa Almadrassatul-nurul- huda ya kijiji cha Mjengo wa Banda shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba, wametakiwa kuepukana na kufanyiana vitendo vya udhalilishaji miongoni mwao, kwani madhara yake ni makubwa.   Hayo yameelezwa leo Novemba 12, 2023 na Msaidizi washeria   wa jimbo la Wawi, Haji Nassor Mohamed, wakati alipokua akitoa taaluma katika madrassa hiyo, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji mpango kazi wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba CHAPO. Alisema zipo njia mbalimbali ambazo mtu humfanyia mwenzake kumpelekea kumuathiri kiakili, kimwili na kijamii ikiwemo kumwita jina baya au kumpiga kipigo cha kuathiri mwili wake. Alisema, zipo aina nyingi za udhalilishaji lakini ambazo hazizungumzwi sana ni kuitana majina mabaya, kuzomeana, kuigizana na kwa sauti au Watoto wenyewe kwa wenyewe kudhalilishaana kingono. ‘’Zipo tabia mbali mbali kwa wanafunzi hasa wakike, yakupigana makofi sehemu za makalio au kw...