CHAPO: ‘WARIPOTINI WAZAZI, WAALIMU, WAJOMBA WANAOTAKA KUWADHALILISHA''
NA MWANDISHI WETU, PEMBA WANAFUNZI wa chuo cha Kur-an cha Kichangani shehia ya Mgogoni Jimbo la Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba, wamekumbushwa kuwaripoti wazazi, waalimu, walezi na watu wengine, wanapoona dalili za wao, kutaka kudhalilishwa . Walieleza kuwa, moja ya dalili hiyo ni mtu huyo kuongeza mapenzi ya kupindukia, kumpa zawadi zisizotarajiwa na kumshika shika sehemu nyeti za mwili wake, ikiwemo kifuani na makalio. Ushauri huo umetolewa na Msaidizi wa sheria, Jimbo la Wawi Fatma Hilali, wakati akizungumza na wanafunzi hao na waalimu, kwenye mkutano wa wazi, wa utoaji elimu, juu ya namna ya kujikinga na majanga yakiwemo ya udhalilishaji. Aliwaambia wanafunzi hao kuwa, dalili nyingine ni kupigwa mabusu sehemu tofauti za mwili, kupewa fedha na hasa na mtu asiyemjua pamoja na kupakatwa. ‘’Wanafunzi mkiona kuna dalili za kawaida, mtu anakushika kwenye mashavu, makalio, kifuani, mbavuni, anakupa pesa na hasa kwa mtu wa nje, pipi toweni taarifa kwa waalim au wazazi,’...