CHAPO: 'WAPENI ELIMU YA KINGA WAZAZI WIZI WA WATOTO'
NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@ JUMUIYA ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’ imewakumbusha wasaidizi wa sheria wilayani humo, kutilia maanani, elimu kwa jamii, juu ya wimbi la wizi wa watoto lililoibuka hivi karibuni. Kauli hiyo imetolewa leo Julai 27, 2024 na Afisa Ufuatiliani na Tathmini kutoka ‘CHAPO’ Wahida Kombo Khamis, kwenye kikao cha mwezi cha kuwasilisha ripoti za elimu na msaada wa kisheria, kilichofanyika ofisini kwao mjini Chake chake. Alisema, pamoja na kuwaelimisha wananchi juu ya udhalilishaji, migogoro ya ardhi, ndoa, wizi, dawa za kulevya pamoja na kuhubiri amani, lakini watilie mkazo, juu ya elimu ya tahadhari ya wizi wa watoto. Alieleza kuwa, ijapokuwa kwa wilaya ya Chake chake halijakua la kutisha jambo hilo, kama ilivyo kwa baadhi ya mikoa ya Tanzania bara, lakini ni vyema, kinga ikaanza kuwekwa. Alifahamisha kuwa, hilo ni miongoni mwa majukumu ya wasaidizi wa sheria, hivyo ni wakati sasa kulieleza kwa upana, ili jamii ifahamu...