TANGAAZO LA UCHUKUAJI NA UREJESHAJI FOMU-UCHAGUZI MDOGO CHAPO

 


TANGAAZO LA UCHUKUAJI NA UREJESHAJI FOMU YA KUGOMBEA NAFASI YA MKURUGENZI -CHAPO

KAMATI ndogo ya Uchaguzi, ikiongozwa na Mwenyekiti wake, Mwanasheria Siti Habib Mohamed, inawatangaazia wanachama wote wa Jumuiya ya Wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’, kua kuanzia tarehe 26.08.2024,  Tume hiyo imeanza kutoa fomu kwa kila mwanachama wa CHAPO, kwa ajili ya uchaguzi mdogo, wa kujaza nafasi ya Mkurugenzi wa CHAPO, ambae alifariki Augost 7, mwaka 2024.

Fomu hiyo, inapatikana Ofisi ya CHAPO, iliyopo mjini Chake chake, kuanzia saa 3:00 asubuhi hadi saa 9:00 jioni kwa siku zote za kazi.

Fomu baada ya kujazwa vyema, kama yalivyo maelekezo, itatakiwa kurejeshwa ofisi ya CHAPO, iliyopo Chake chake Pemba, sio zaidi ya tarehe 29.08.2024, saa 8:40 mchana.

Ikiwa na vielelezo vifuatavyo:

a)    Picha moja ya Mgombea, iliyopigwa hivi karibuni,

b)    Ada ya fomu y shilingi 2,500/= (Shilingi Elfu Mbili Mia Tano tu)

c)    Nambari ya usajili ya uanachama.

d)    Saini ya Mdhamini wako.

 

PIA fomu hiyo inapatikana kupitia. FOMU YA KUOMBA KUGOMBEA NAFASI YA MKURUGENZI CHAPO (chapo24.blogspot.com)

 

NB: ANGALIZO KWA WAGOMBEA

 -Fomu itakayojazwa kwa kalamu isiyokuwa BULUU, AU kujazwa kwa herufi NDOGO, kukozeshea maadishi au isiyokuwa na ADA haitozingatiwa na Tume.

Kwa maelezo zaidi, wasiliana na Mwenyekiti wa Tume +255777679747 au Katib +255778921827

 

Comments

Popular posts from this blog

AFISI YA MWANASHERIA MKUU ZANZIBAR YAKUSANYA MAONI SHERIA YA MSAADA WA KISHERIA

MKURUGENZI HANIFA, AWAUMA SIKIO WANANCHI WAWI HAKI ZA BINAADAMU

‘WANANCHI HAWANA MAMLAKA YA KUONDOSHA UHAI WA MTU’