WAJUMBE SHEHIA MVUMONI WAPIGWA MSASA ELIMU YA KISHERIA
NA MWANDISHI WETU, PEMBA WAJUMBE wa sheha wa shehia ya Mvumoni wilaya ya Chake chake, wameelezwa kuwa, suala la haki za binaadamu sio la kuomba, bali ni haki ya kila mmoja, kwa ubinaadamu wake. Mkurugenzi wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilayani humo ‘CHAPO’ Mohamed Hassan Abdall, aliyasema hayo leo Disemba 7, 2025 wakati akiwasilisha mada ya haki za binaadamu, kwa wajumbe hao, kwenye mafunzo ya siku moja. Alisema, haki za binaadamu, ni haki zote anazostahiki mtu, kwa sababu ya kuwepo kwake duniani, ikiwemo uhai, matibabu, afya, elimu, utaifa na uzalendo. ‘’Niwaombe sana wajumbe wetu wa shehia ya Mvumoni, kwanza elimu hii mkawafikishie na wingine, maana haki za binaadamu ni zote,’’alieleza. Akizungumzia faida za kufanya sulhu kwa kesi za madai kama vile, huduma za mke, watoto, migogoro ya ardhi, mirathi na madeni, alisema inaondosha visasi. Alifahamisha, kuwa ndio maana, wamempeleka msaidizi wa sheria katika eneo lao...