MKURUGENZI 'CHAPO' AWAVUTIA PUMZI WAJUMBE WATORO WA VIKAO
NA HAJI NASSOR, PEMBA::: MKURUGENZI wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’ Nassor Bilali Ali, ameelezea kusikitishwa kwake na baadhi ya watendaji wa jumuiya hiyo, kukumbwa na dharura kila panapoitishwa vikao. Alisema, wapo baadhi ya watendaji sasa wamekuwa ndio ugonjwa wao usio na tiba wa kutohudhuria vikao, jambo ambalo kwa baadhi ya wakati, hurejesha nyuma mipango na mikakati yao. Mkurugenzi huyo ameyasema hayo, Novemba 5, mwaka 2022, ofisini kwake mjini Chake chake, wakati akizungumza na watendaji wake, kwenye kikao cha robo ya nne ya mwaka. Alisema vikao ni sehemu muhimu ya kutengeneza, kuunda au kuamua jambo husika kwa maslahi ya wananchi wa wilaya ya Chake chake, sasa ikiwa kuna wajumbe ni wagonjwa kwa dharura wanaweza kukwamisha jitahada. Alisema kuanzia sasa ‘CHAPO’ itakuwa wakali kwa wajumbe watoro na wasiopenda kufuata wakati wa vikao husika, kwani kinyume chake, wanaweza kukwamisha baadh...