Posts

Showing posts from April, 2024

'WALINDENI WATOTO NA WATUMIAJI WA DAWA ZA KULEVYA'

Image
  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI wa kijiji cha Birikau shehia ya Michungwani wilaya ya Chake chake Pemba, wametakiwa kuwalinda watoto wao, kwani watumiaji, wasafirishaji na waingizaji wa dawa za kulevya, wamekuwa wakiwatumia watoto, katika kufanikisha malengo yao. Ushauri huo umetolewa April 30, 2024 na Askari kutoka Jeshi la Polisi wilaya ya Chake chake, anayezifanyia kazi shehia za Wesha, Michungwani na Ndagoni wilayani humo Khamis Ali Khamis, wakati akizungumza na wananchi, kwenye mkutano wa wazi. Alisema, kwa sasa watumiaji na wasafirishaji wamekuwa wakiwatumia watoto, wakijua kuwa, kisheria hawashatakiwa na wakati mwingine hawawezi kupekuliwa. Alieleza kuwa, taarifa zipo zinazoenesha kuwa, sasa watoto wamekuwa wakitumiwa na watumiaji, wasaambazaji wa dawa za kulevya, baada ya mitego ya kuwatumia watu wazima kugundulika. ‘’Wazazi wa kijiji ch Birikau, kuweni makini mno na wasambaazaji, watumiaji, wauzaji na waingizaji wa dawa za kulevya, sasa wamehamishia kazi hiy...

'CHAPO' YAZINDUA VILABU VYA KUPINGA UDHALILISHAJI MABARAZA YA WATOTO

Image
    NA HAJI NASSSOR, PEMBA@@@@ AFISA Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto wilaya ya Chake chake Salma Khamis Haji, amewataka watoto wilayani humo, kutoa taarifa, pindi wanakapoona viashiria vya ukatili na udalilishaji dhidi yao, ikiwemo kuanza kuchezewa sehemu zao za siri. Hayo ameyasema leo April 28, 2024, skuli ya Maandalizi Madungu, wakati akieleza wajibu wa mabaraza hayo, kwenye mkutano wa uzinduzi wa vilabu vya kupinga ukatili na udhalilishaji wa kijinsia, kupitia mradi wa upatikanaji haki, unaoendesha na Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake ‘CHAPO’. Alisema moja ya malengo ya vilabu hivyo, ni kuwawezesha watoto hao, kutetea mambo yanayohusu, huku jambo la mwanzo likiwa ni kutokukaa kimnya wanapoona viashiria vibaya kwao. Alieleza kuwa, kiashiria kimoja wapo ambacho wanatakiwa kukiripoti ni kuanza kuchezewa sehemu za miili yao, kupewa zawadi na fedha zisizo na sababu maalum, pamoja na kuitwa maeneo yasio rasmi (vichakani). Alieleza kuwa, wapo watu ...

ALIYEUPASUA MPIRA WA WATOTO WESHA ULIOTOLEWA NA CHAPO AAHIDI KUULIPA

Image
  NA HAJI NASSOR, PEMB A@@@@ MWANAMKASI Mikidadi Maeda (38) wa shehia ya Wesha wilaya ya Chake chake, amekubali ushauri wa wasaidizi wa sheria wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilayani humo, ‘CHAPO’ kulipa gharama za mpira mmoja wa miguu, alioupasua baada ya kumgonga kwa bahati mbaya, wakati timu ya ‘kaza buti’ inyomilikiwa na baraza la watoto la shehia hiyo, walipokuwa wakifanya mazoezi. Mpira huo awali, ulikabidhiwa kwa uongozi wa baraza hilo ukitoka CHAPO, Machi 20, mwaka huu, kwa ajili ya timu hiyo, ikiwa ni ahadi ya wasaidizi wa sheria, walioitoa kwa watoto hao, mwishoni mwa mwaka jana. Kwenye kikao cha sulhu kilichofanyika nyumbani kwa sheha wa shehia ya Wesha, mwananchi huyo alikiri kosa la kujichukulia sheria mikononi, mara baada ya tukio hilo la yeye kugongwa mpira wa uso. Alisema siku ya tukio hilo, alikuwa nyumbani kwake, kando kando ya uwanja huo, wakati akiwa kwenye harakati zake, alishtukia mpira ukienda usoni mwake, na kumsababisha maumivu, jambo ambalo li...