WANANCHI 422,908 WAFIKIWA KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA YA MAMA SAMIA
NA HAJI NASSOR, UNGUJA@@@@ WANANCHI 422,908 wakiwemo wanawake 209,185 na wanaume 213,723 wamefikiwa na elimu na msaada wa kisheria, kupitia kampeni ya msaada wa kisheria ya Mama Samia, iliyomalizika hivi karibuni Zanzibar. Kampeni hiyo, iliendeshwa katika mikoa yote mitano ya Zanzibar, inayojumuisha wilaya 11, ambapo miongoni mwao kati ya waliofikiwa, ni wanawake, watu wenye ulemavu, vijana, wazee na wanafunzi. Hayo yalielezwa leo Julai 16, 2025 na Mwanasheria Mkuu wa serikali ya Zanzubar, Mwinyi Talib Haji, kwenye hutuba yake, iliyosomwa kwa niaba yake na Naibu Mwanasheria mkuu Shaaban Ramadhan Abdalla, kwenye kilele cha maadhimisho ya jukwaa la tano, kilichofanyika Michenzani Mall. Alisema, kwa takwimu hiyo na kazi iliyofanywa, inadhahirisha umoja na mshikamano, unaosababishwa na uwepo wa Muungano wa Tangayika na Zanzibar. Alieleza kuwa, serikali inafurahishwa mno kuona wananchi walio wengi na wanyonge, wanaendelea kupata msaada, ushauri na elimu ya kisheria bila ya ...