Posts

Showing posts from March, 2024

CHAPO YAPOKEA WASAIDIZI WA SHERIA WAPYA, YAWAPA NENO

Image
  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ JUMUIYA ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba CHAPO, imewapokea wasaidizi wa sheria wapya na kuwahakikishia ushirikiano wa hali ya juu, ili kufikia malengo ya kuihudumia jamii, wilayani humo. Hayo yalielezwa leo Machi 30, 2024 na Mkurugenzi wa ‘CHAPO’ Nassor Bilali Ali, wakati wa ukaribisho na mapokezi ya wasaidizi wapya watatu wa sheria, kutoka shehia za Michungwani, Kibokoni na Mgelema, hafla iliyofanyika ofisi ya CHAPO, mjini Chake chake. Alisema, C HAPO inafarajika mno kuona sasa inaongeza idadi ya wasaidizi wa sheria 21, kutoka 18 wa awali, jambo ambalo linaendelea kupunguza ukakasi kwa shehia 11, zitakazobakia bila ya kuwa na wasaidizi wa sheria, kati ya zote 32 za wilaya hiyo. Alieleza kuwa, wasaidizi hao wa sheria wapya, watapewa kila aina ya ushirikiano, wakati huu wa miezi mitatu wakiwa kwenye majaribio na hata baada ya kumaliza na kuanza kazi rasmi shehiani mwao. Mkurugenzi Nassor alifafanua kuwa, wananchi wa vijiji wana...

CHAPO YAMALIZA SIUTAFAHAMU MATUMIZI UWANJA WA SOKA WESHA

Image
  NA ABDALLA MBAROUK, PEMBA @@@@ WASAIDIZI wa sheria kutoka wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’ wamemaliza siutafahamu ya matumizi ya uwanja wa mpira wa miguu, baina ya timu ya watoto ya Baraza la watoto la shehia ya Wesha na wachezaji wa vilabu vikubwa shehiani humo. Itakumbukwa kuwa, Disemba 17, mwaka 2023, wasaidizi hao wa sheria, walipokea lalamiko la kusitishwa kwa matumizi ya uwanja uliopo Wesha kwa sheha, timu ya kazabuti inayomilikiwa na baraza la watoto la shehia hiyo, wakielezwa kuwa, hawana haki ya matumizi ya uwanja huo. Ambapo baada ya malalamiko hayo, wasaidizi wa sheria kutoka CHAPO, wakiongozwa na Msaidizi wa sheria mwenyeji wa shehia ya Wesha, Khadija Said Khalfan, waliahidi kulitafutia ufumbuzi lalamiko hilo. Msaidizi wa sheria huyo akiwa na wenzake watatu, waliahidi kukutana na uongozi wa vilabu vikubwa vinavyotumiwa uwanja huo, ili kuona na timu ya kaza buti ya baraza la watoto la shehia ya Wesha, nao wanautumia uwanja huo kufanya mazoezi. Ndipo le...