MWAKILISHI WAWI ABARIKI CHAPO KUANZISHA DARASA LA SHERIA KWA WANANCHI
NA HAJI NASSOR, PEMBA:: MWAKILISHI wa Jimbo la Wawi Bakar Hamad Bakar, ameunga mkono, wazo la wasaidizi wa sheria Jimbo la Wawi, la kutaka kuanzishwa darasa maalum la kutoa elimu ya sheria, kwa wananchi wa shehia ya Wawi jimboni humo. Alisema, wazo la wasaidizi hao wa sheria, kutaka kuanzisha darasa maalum, ni jambo la msingi, kwani elimu waliyopatiwa wao, itasambaa kwa upana. Mwakilishi huyo aliyasema hayo, Febuari 19, 2023 wakati akizungumza na uongozi wa shehia ya Wawi, kwenye kikao maalum cha maandalizi ya darasa hilo. Alisema, wananchi wanahitaji kupata elimu ya kujua haki na wajibu wao kwa jamii, samba mba na kupata uwelewa wa mambo ya kisheria. ‘’Kwanza niunge mkono wazo ambalo wenzetu hawa wasaidizi wa sheria Jimbo la Wawi, wameliwaza na mimi nitaunga mkono kwa hali na mali, ili kufanikisha darasa hilo,’’alieleza. Katika hatua nyingine, Mwakilishi huyo wa Jimbo la Wawi aliwataka wasaidizi hao wa sheria, kuhakikisha darasa hilo linakuwa endelevu, kwa kundi jing...