LSF: YATOA USHAURI WA BURE KWA JUMUIYA ZA WASAIDIZI WA SHERIA PEMBA
NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MRATIBU wa taasisi ya ‘LSF’ kanda ya Zanzibar Hamisa Bakar Hamad, amesema kama jumuiya za wasaidizi wa sheria, hazikuungana wakati zinapotekeleza miradi, inaweza kuwa jambo gumu kufikia malengo ya miradi hiyo kwa jamii. Alisema, jumuiya hizo zote ni zinamalengo yanayofanana ya kuisaidia jamii, hivyo ili kufikia malengo hayo hazinabudi, kushirikishana na kufanyakazi kwa pamoja. Mratibu huyo wa kanda aliyasema hayo, ofisini kwake Madungu mjini Chake chake, kwenye mafunzo ya siku mbili kwa wanaasasi za wasaidizi wa sheria, katika kuutambulisha mradi wa suati ya mwanamke. Alieleza kuwa, kama jumuiya zinaelekea kuisaidia jamii, hakunabudi moja inapotekeleza mradi husika, kushirikiana na nyingine. Alifahamisha kuwa, sio busara kuona taasisi zilizojirani, moja inatekeleza mradi ambao mwenzake alishautekeleza miezi kadhaa iliyopita. ‘’Kwa mfano kama ‘CHAPO’ anatekeleza mradi wa afya ya mama, ni vyema na jirani yake ‘MDIPAO’, kuelekezana ili kusaidiana ushauri na...