Posts

Showing posts from July, 2022

WANANCHI PUJINI WATAJA VYANZO VYA MIGOGORO YA ARDHI

Image
  NA HAJI NASSOR, PEMBA WANANCHI wa shehia za Pujini, Mfikiwa na Dodo mkoa wa kusini Pemba, wamesema moja ya sababu inayochangia uwepo wa migogoro ya ardhi katika jamii, ni ucheleweshwaji wa mirathi kwa wahusika. Walisema, wapo baadhi ya wanaume katika familia, mara baada ya kifo cha mrithiwa, huikumbatia mirathi na wakati mwengine hadi kuwapa lugha za vitisho warithi wenzao, na mwisho huzaliwa migogoro inayozuilika. Wakichangia mada ya usuluhishi wa migogoro ya aradhi, kwenye mafunzo ya kuzuia migogoro kwenye maeneo ya uwekezaji na kufanyika kituo cha ubunifu wa kisayansi Pujini, wananchi hao walisema, hilo bado ni tatizo. Walieleza kuwa, wanaume hao wamekuwa wakipuuzia maandikiko matakatifu yanayohimiza suala la kulipa kipaumbele urithi, mara baada ya muhusika kufariki. Mmoja kati ya wananchi hao Abdallah Kombo, alisema utamaduni wa kumilikiwa mirathi na mtu mmoja, na kuwaacha wengine pembeni, huzaa migogoro mfano kama ya ardhi. ‘’Moja ya sababu ya uwepo wa migogoro n...

MKURUGENZI CHAPO, AWAPA USHAURI WA BURE MASHEHA

Image
  IMEANDIKWA NA KHADIJA NA HAJI- CHAPO::: MKURUGENZI wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheri wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’ Nassor Bilali Ali, amewataka masheha, kutayarisha kamati za usuluhishi wa migigoro ya ardhi, zinazokubalika na jamii, ili iwe rahisi wakati wa utendaji wao wa kazi. Alisema, moja ya jukumu la kamati hizo hapo baadae, ni kusikiliza migogoro ya ardhi, na kuota ushauri kwa ajili ya kupatikana kwa sulhu, hivyo lazima wachugue wajumbe wanaokubalika katika jamii. Ushauri huo, ameutoa jana wakati akizungumza, kwenye uzinduzi wa mradi wa Kujenga uwelewa kwa jamii, katika kuzuia migogoro itokanayo na matumizi ya ardhi ya uwekezaji, na kufanyika skuli ya Pujini wilaya ya Chake chake. Alisema, kamati hiyo itaundwa na wajumbe, na kisha kupewa elimu ya utatuzi wa migogoro na hata baada ya mradi huo kukamilika, itatakiwa kuendelea kufanyakazi kwa jamii. ‘’Masheha ni watu wenye uwelewa mkubwa, hivyo natamani sana kuona wakati ukifika, tupate wajumbe wa kamati wanaoku...

CHAPO, FUNDATION LEO PUJINI KUZINDUA MRADI WA KUZUIA MIGOGORO YA ARDHI

Image
  NA HAJI NASSOR, PEMBA JUMUIYA ya Wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’ leo Julai 23, mwaka huu, inatarajia kuzindua mradi wa mwezi mmoja wa ‘Kujenga uwelewa kwa jamii katika kuzuia migogoro itokanayo na matumizi ya ardhi, kwa shuguli za uwekezaji Pemba. Mradi huo ambao unatarajiwa kumalizika Augosti 30, mwaka huu, unatarajiwa kutekelezwa katika shehia tatu za Mfikiwa, Pujini na Dodo ukifadhiliwa na tasisi ya ‘the foundation for Civil Society ya Tanzania’. Akitoa taarifa ya namna ya utekelezaji wa mradi huo mbele ya watendaji wa CHAPO, kwenye kikao kilichofanyika ofisini kwao Chake chake, Mkurugenzi wa ‘CHAPO’ Nassor Bilali Ali, alisema upatikanaji wa mradi huo, ni faraja kwao. Alisema, ni sahihi katika maeneo yenye uwekezaji suala la uwepo wa migogoro ya ardhi, baina ya wananchi na wawekezaji huwa haliepukiki, na ndio maana wametafuta mradi huo. Alieleza kuwa, CHAPO kwa kushirikiana na wafadhili wao, watakuwa na mikutano miwili ya ndani, na mikutano mitatu ya wa...

CHAPO YATAMBULISHA MRADI KWA WATENDAJI WAKE

Image
  NA HAJI NASSOR, PEMBA JUMUIYA ya Wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’ Julai 23, mwaka huu, inatarajia kuzindua mradi wa mwezi mmoja wa ‘Kujenga uwelewa kwa jamii katika kuzuia migogoro itokanayo na matumizi ya ardhi, kwa shuguli za uwekezaji Pemba. Mradi huo ambao unatarajiwa kumalizika Augosti 30, mwaka huu, unatarajiwa kutekelezwa katika shehia tatu za Mfikiwa, Pujini na Dodo ukifadhiliwa na tasisi ya ‘the foundation for Civil Society ya Tanzania’. Akitoa taarifa ya namna ya utekelezaji wa mradi huo mbele ya watendaji wa CHAPO, kwenye kikao kilichofanyika ofisini kwao Chake chake, Mkurugenzi wa ‘CHAPO’ Nassor Bilali Ali, alisema upatikanaji wa mradi huo, ni faraja kwao. Alisema, ni sahihi katika maeneo yenye uwekezaji suala la uwepo wa migogoro ya ardhi, baina ya wananchi na wawekezaji huwa haliepukiki, na ndio maana wametafuta mradi huo. Alieleza kuwa, CHAPO kwa kushirikiana na wafadhili wao, watakuwa na mikutano miwili ya ndani, na mikutano mitatu...

HATA WALIOPO KIZUIZINI WANA HAKI YA KUPATA MSAADA WA KISHERIA

Image
  NA HAJI NASSOR, PEMBA:::- ‘’WATU wote ni sawa mbele ya sheria, na wanayo haki, bila ya ubaguzi wowote, kulindwa na kupata haki sawa mbele ya sheria,’’ ndivyo inavyofafanua Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984. Maelekezo hayo utayafuma mara ukiifungua Katiba hiyo, kwenye kifungu chake cha 12 (1), ingwa suala la kupata msaada wa kisheria, haliguswi moja moja, lakini msingi wa hilo upo. Ndio maana hapo sasa, kwa kuzingia msingi huo wa sheria mama yaani Katiba (ground norm),  tunaweza kusema kwa kinywa kipana kuwa, haki ya kupata msaada wa kisheria unamgusa kila mmoja. Nikuulize, msingi wa usawa mbele ya sheria kwenye kifungu hicho cha 12, kweli unaweza kuwa na maana, iwapo wenzetu walioko kizuizini, ambao pia uhuru wao umedhibitiwa wasiwe na haki ya kupata msaada wa kisheria? Kwa hakika, tena kwa jicho hata lisilokuwa na uwana sheria utagundua kuwa, haki ya kupata msaada wa kisheria unawahusu, hata walioko kizuizini. AZIMIO LA HAKI ZA BINADAMU Haki ya mtu kuwa huru, na kutokamatwa ...

RC KUSINI PEMBA: AIPONGEZA KAMATI MAANDALIZI SIKU YA MTOTO AFRIKA -PEMBA

Image
    NA HAJI NASSOR, PEMBA:::- MKUU wa Mkoa wa kusini Pemba Mattar Zahor Massoud, amesema ameridhishwa na matayarisho ya awali, yaliyofanywa na wajumbe wa Kamati maalum ya maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika, kisiwani humo. Alisema, kamati hiyo imeibua jambo kubwa la kutaka kufanya maadhimisho hayo, na kujipanga kwa kufanya shughuli mbali mbali, kabla na wakati wa kilele chenyewe ambacho ni Juni 16, mwaka huu. Alisema ameridhishwa na mpango huo wa maadhimisho na kuahidi kushirikiana nao, hadi kukamilika kwake siku ya kilele hicho kinachotarajiwa kufanyika uwanja wa Gombani. Mkuu huyo wa mkoa aliyasema hayo Juni 11, 2022 ofisini kwake Chake chake, wakati akizungumza na wajumbe wa kamati hiyo, waliofika ofisini kwake, kuwasilisha mpango pendekezwa wa kilele hicho. Alisema, suala la kuwashirikisha watoto ambao ni wanafunzi na kuwaandalia michezo mbali mbali kama ushindani kwenye elimu, ni jambo linalofaa kuungwa mkono. ‘’Kwanza niwapongeze wajumbe wa kamati hii, kwa uamuzi wao ...

MKURUGENZI CHAPO AWAKARIBISHA WASAIDIZI WA SHERIA WAPYA CHAKE CHAKE

Image
  NA HAJI NASSOR, PEMBA:::- MKURUGENZI wa Jumuiya ya Wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake 'CHAPO' Nassor Bilali Ali, amewataka wasaidizi wa sheria wapya, wa majimbo ya wilaya hiyo, kufanyakazi kwa bidi, ili kuisaidia jamii, kupunguza matendo ya udhalilishaji. Alisema, jamii inakabiliwa na majanga kadhaa pamoja na utumiaji wa dawa za kulevya, migogoro ya ndoa, ardhi na matunzo ya watoto, hivyo ni wajibu wao kuona hayo yanapungua. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, baada ya kuwapokea wasaidizi hao wa sheria, alisema amefarajika kuona, Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria, imewapa mafunzo vijana hao. Alisema, moja ya eneo la Zanzibar ambalo haliko salama na majanga mbali mbali ni wilaya ya Chake chake, hivyo wasaidizi hao wa sheria, wanayokazi ya kufanya ndani ya jamii. ‘’Karibuni sana kwenye jumuiya yetu hii, na sisi tumefarajika kuona, tumepata damu changa ya kupambana na majanga mbali mbali, ili tuwe na taifa lenye amani,’’alieleza. Aidha Mkurugenzi huyo, alisema wa...