CHAPO: ‘WAZAZI TENGENI MUDA KUZUNGUMZA NA WATOTO WENU’

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

 

WAZAZI na walezi wa kijiji ch Jamvini shehia ya Ndagoni, wilaya ya Chake chake Pemba, wametakiwa kutenga muda wa kukaa na watoto wao, ili kuwahoji yaliotokezea mchana mzima, kwa lengo kubaini ikiwa wameanza kufanyiwa vitendo vya udhalilishaji ama laa.

 

Ushauri huo umetolewa Novemba 25, 2023 na Masaidizi wa sheria Jimbo la Ziwani, shehia ya Wesha Khadija Said Khalfan, wakati akizungumza na wazazi na walezi, pamoja na watoto wao, wa kijiji cha Jamvini, ikiwa ni mikutano ya kutoa elimu ndani ya siku 16 za kupinga ukatili na udhalilishaji wa wanawake na watoto.

 

Alisema, njia moja wapo ya kubaini, iwapo mtoto ameanza kubadili tabia na hasa kwenye vitendo vya udhalilishaji, ni wazazi kutenda muda, wa kukaa na watoto hao.

 

Alieleza kuwa, hipendezi kuona wazazi hao, wanaelekeza nguvu zao zaidi katika kutafuta maisha pekee, bali waelewa kuwa, sasa ulimwengu umebadilika na yapo majanga ambayo huwakumba watoto.

 



Msaidizi huyo wa sheria, alifafanua kuwa, kupitia mazungumzo ya watoto, wanapokaa na wazazi ama walezi wao, wanaweza kugundua ikiwa wameanza kutekwa kiakili na wadhalilishaji.

 

‘’Ni kweli maisha yamepanda juu, na wapo wazazi wanatoka alfajiri na kurudi nyumbani usiku, lakini ili kukabiliana na majanga haya, tujitengee muda kukaa na watoto wetu,’’alisisitiza.

 

Katika hatua nyingine, Msaidizi huyo wa sheria, alisema wao wapo kwa ajili ya kuwasadia wananchi, ikiwemo kutoa elimu, ushauri na msaada wa kisheria, bila ya malipo.

 

‘’Mnapoona kuna kitu kinawatatiza kisheria, tutafuteni ofisi yetu ipo Chake chake mjini mkabala na tume za uchaguzi, na tunatoa msaada wa kisheria bila ya malipo,’’aliafafanua.

 

Kuhusu siku16 za kupinga ukatili na udhalilishaji, aliitaka jamii kila mmoja, kuwa mlinzi kwa mwenzake, ili kuhakikisha hakuna anayezifanyia sulhu kesi za udhalilishaji.

 

Kwa upande wake Mkaguzi Msaidizi wa Polisi anayefanyakazi katika shehia ya Ndagoni na Wesha Khamis Asli Khamis, aliikumbusha jamii, juu ya wajibu na haki yao ya kushirikiana na vyombo vya sheria, ikiwa wana nia ya kutokomeza uhalifu.

 



Alieleza kuwa, jamii inaweza kushirikiana kwa njia kadhaa ikiwemo ya kutoa ushahidi, kuonesha mtuhumiwa alipo, kutoa elimu ya athari ya uhalifu pamoja na kuzifikisha kesi katika vyombo vya ulinzi na usalama.

 

Aidha askari huyo shehia, aliwataka watoto kutoa taarifa pindi watakapoona dalili za kutaka kudhalilishwa hata iwe kwa baba, kaka, mjomba, mwalimu wa skuli au mtu mwingine wa familia.

 

‘’Hata kama anayekushika shika sehemu zako za siri ni mwalimu au kaka, toa taarifa kwa mama au kwa mtu mwingine unaemjua, ili nae achukuliwe hatua, maana hicho ndio chanzo cha kutaka kufanyiwa udhalilishaji,’’alieleza.

 

Nae Mratibu wa wanawake na watoto shehia ya Ndagoni Shuwarika Ali Mohamed, alisema hatomuhurumia mtu yeyote, ambae atakua na kesi ya jinai, na kisha kuanza taratibu za kuzisuluhisha.

 


‘’Ipo tabia kwa baadhi ya watu, wanaweza kujua mtoto wake amedhalilishwa, basi wakakimbilia kwenye ufungaji wa ndoa, na wasipofahamiana huko, huja kwangu, kwamba kesi tuishughulikie lakini nasema naanza na wewe kwanza kukuripoti sehemu husika,’’alieleza.

 

Hata hivyo, amewakumbusha wananchi kuendelea kuwatumia wasaidizi wa sheria, kwani wana nafasi kubwa katika suala la kuelimisha jamii, juu ya umuhimu wa kuzilinda haki za binaadamu.

 




ia ya wasadizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba CHAPO, imo katika kampeni maalum ya kutoa elimu ya kupinga ukatili na udhalilishaji, ndani ya siku 16 za kupinga ukatili, kwa kupita katika shehia mbali mbali za wilaya hiyo.

 

 MWISHO

 

Comments

Popular posts from this blog

AFISI YA MWANASHERIA MKUU ZANZIBAR YAKUSANYA MAONI SHERIA YA MSAADA WA KISHERIA

MKURUGENZI HANIFA, AWAUMA SIKIO WANANCHI WAWI HAKI ZA BINAADAMU

‘WANANCHI HAWANA MAMLAKA YA KUONDOSHA UHAI WA MTU’