CHAPO: ‘’WANAFUNZI JIEPUSHENI KUFANYIANA UDHALILISHAJI WENYEWE’’
NA ASHA ABDALLA, PEMBA
WANAFUNZI wa Almadrassatul-nurul-
huda ya kijiji cha Mjengo wa Banda shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba,
wametakiwa kuepukana na kufanyiana vitendo vya udhalilishaji miongoni mwao, kwani
madhara yake ni makubwa.
Hayo yameelezwa leo Novemba 12, 2023 na Msaidizi washeria wa jimbo la Wawi, Haji Nassor Mohamed, wakati
alipokua akitoa taaluma katika madrassa hiyo, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji
mpango kazi wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba CHAPO.
Alisema
zipo njia mbalimbali ambazo mtu humfanyia mwenzake kumpelekea kumuathiri
kiakili, kimwili na kijamii ikiwemo kumwita jina baya au kumpiga kipigo cha
kuathiri mwili wake.
Alisema,
zipo aina nyingi za udhalilishaji lakini ambazo hazizungumzwi sana ni kuitana
majina mabaya, kuzomeana, kuigizana na kwa sauti au Watoto wenyewe kwa wenyewe
kudhalilishaana kingono.
‘’Zipo
tabia mbali mbali kwa wanafunzi hasa wakike, yakupigana makofi sehemu za
makalio au kwenye kifua, na kwaupande wanafunzi wanaume kufanyiana michezo ya
kwenye vichaka, na kisha kulipiziana kwa mfumo wa kudhalilishana,’’alieleza.
Akizungumzia
kuhusu njia chafu ambazo mtoto anaweza kukubali kudhalilishwa ni kwa baadhi ya
wazazi na walezi, kuwaachia watoto wao kuangali michezo kwenye tv au kuchezea
simu zao na kuona picha zilizo nje ya maadili yao.
‘’Katika
baadhi ya nyumba wazazi wanadhani kuwapenda watoto wao, ni kuwaachia tv na kuweka
michezo watakayo, bila ya kujali athari ya wanachokiangalia,’’alifafanua.
Hata
hivyo, amewakumbusha kuwa, wanapoona wenzao au wao wenyewe kuna viashiria vya
kutaka kufanyiwa vitendo vya udhalilisaji, wasisite kutoa taarifa aidha kwa
waalimu, wazazi, walezi au uongozi wa sheria.
Kwa
upande wa Mwanafunzi wa madrasa hiyo Rufaida Abdalla Omar, alitaka kujua kuhusu
wanawake kwa wanawake, kupigana mabusu bila yamwenyewe kuridhiana, ikiwa hilo
ni kosa kisheria.
Nae mwanafunzi Hashiri Kombo Hamad, alitaka
kujua kutoka kwa Msaidizi huyo wa sheria, juu ya suala ka kuchungulia ndani mwa mtu (kupiga bodi), ikiwa linaingia katika
makosa ya udhalilishaji.
‘’Maana
wapo watu wanapiga bodi katika nyumba za watu, lakini sioni wakichukuliwa
hatua, na je hili nalo ni kosa katika yale ya udhalilishaji,’’aliuliza mwanafunzi
huyo.
Kwa
upande wake mwanafunzi Nihlat Mohamed Abass, alita kuwepo kwa muongozo maalumu,
kwa waalimu wa madrssa juu ya idadi ya bakora kwa wanafunzi kwa aina ya kosa alilotenda.
‘’Isiwe
mwalimu anaamua yeye mwenyewe, juu ya idadai, sasa ni vyema kuwepo kwa muongozo
husika wa waalimu juu ya adabu hiyo kwa wanafunzi wao,’’alieleza.
Nae
mwalimu mkuu msaidizi namba mbili wa madrasa hiyo sheikh Juma Khamis Ali, alisema mpango wa serikarekali
wa kuanzisha wasaidizi wa sheria, unaleta tija kwa jamii.
Alieleza
kuwa, elimu iliyotolewa katika madarassa yake, ni mzuri na imekuja wakati
mwafaka, kwani vitendo hivyo vipo kwa wingi katika jamii yao.
Kwa
upande wake Mkuu wa madrassa hiyo sheikh Mohamed Omar Mohamed, alisema elimu
kama hiyo inafaa kuendelezwa kila baada ya muda, ili watoto wazinduke.
‘’Hapa
madrassa wanaelimishwa kila baada ya muda, lakini tukipata na wasaidizi wa sheria
wakipita, huwa inatusaidia sisi ulezi,’’alieleza.
Aidha
aliitaka CHAPO, kuendelea kuzitembelea madrassa nyingine, ili kukutana na
watoto hao na kuwapa elimu kama waliyopewa wao.
Mdarassa
hiyo iliyoanzishwa na marehemu mwalimu Abass
Hamad Mjaku mwaka 1980, ikiwa na awanafunzi 20, ambapo kwa sasa ina
waalimu watatu, na wanafunzi 130, wakiwemo wanaume 70 na wanawake 60.
Mwisho







Comments
Post a Comment