WANAFUNZI 300 WAFIKIWA NA ELIMU YA HEIDH SALAMA PEMBA

 


AMINA AHMED, PEMBA.

JUMLA  ya wanafunzi wakike  300  wa Skuli za Sekondari Msuka na Chambani Kisiwani Pemba  wamepatiwa  Elimu juu ya  mafunzo ya Hedhi Salama, Ukatili wa kijinsia, pamoja na haki ya Hedhi salama  kwa Mwanafunzi wa Kike. 

 Wanafunzi 233 kati ya hao wamepatiwa  taulo za Kike  zenye uwezo wa kudumu miaka miwili  kutoka   ikiwa ni  shamra shamra za kuadhimisha siku ya Wanawake Duniani inayoadhimishwa kila ifikapo  tarehe 8  Mwezi wa 3 Duniani kote.  

 Msaada wa  taulo hizo kwa Wanafunzi hao uliotolewa na Shirika lisilo la Kiserikali la Smile for Community   ni katika utekelezaji wa Mradi wake wa Run for Binti Marathon, ambao umefadhiliwa na Shirika la Msaada  wa Kisheria Legal Services Facility unaotekelezwa kwa  LSF na kufanya kazi kwa kushirikana na   Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia wizara ya  Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto ,   Maisha Bora Faundation ZMBF, Taasisi ya Weza, pmojana Taasisi ya Waja Mama. 

 Akizungumza na  mwandishi wa habari hizi mara baada ya kumaliza kutoa  Elimu kwa Wanafunzi hao  Afisa Mradi kutoka Shirika la Smile For Community  Anet Kiao  alisema kuwa lengo la kutoa Elimu juu ya suala hilo  ni  kuhakikisha Wanafunzi wakike waliopo Maskulini  wanakuwa salama wanapokuwa katika kipindi cha Hedhi. 



 Alisema suala hilo litawafanya Wanafunzi wa kike kuendelea vyema na Masomo bila kupata usumbufu utakaowapelekea kushindwa kufanya vizuri katika Masomo yao na badala yake waweze kuedelea kubaki skuli kuendelea na Masomo yao. 

"Lengo la kugawa Taulo hizi kwa wanafunzi wakike ambao wameshafikia umri wa balehe ni kuona wanaondokana na usumbufu  wanaokumbana nao wakati wa Hedhi, pale wanapokuwa Skuli ambao kwa namna moja ama nyengine hupelekea kukatisha Masomo yao au kushindwa kufanya vizuri Darasani wanapokuwa katika hali hiyo kupitia Elimu hii tuliyoitoa kwa wanafunzi hawa watajua  sasa nini wafanye wanapokumbana na suala hili", alisema. 

Akitoa Elimu ya  Kisheria kwa Wanafunzi hao Alphonce  Mbarambe Gura  Mwanasheria kutoka  taasisi ya Legal Service  Facility Zanzibar  aliwataka Wanafunzi hao kutokaa kimya  wanapokumbana  na changamoto yeyote inayotokana na Hedhi  kwa vile suala hilo linatambulikana  kikatiba  kama ni haki ya Msingi kati ya  Haki za Binaadamu kwa vile suala  hilo linagusa moja kwa moja utu wa Wanafunzi hao wakike.  

"Lazima suala la Hedhi Salama liangaliwe kwa upana wake hivyo ni lazima Watoto wakike wenyewe  muweze kujua ni jinsi gani suala la hedhi Salama ni muhimu kwenu, mna haki ya kupata vifaa vya kujisitiri kwa gharama nafuu ambavyo ni salama , kupata Mazingira wezeshi Skuli na Nyumbani ya kubadilishia nguo maji  ya  Salam kwa vyovyote hivi munahaki ya kudai  endapo mtakuwa Skuli  ama Majumbani", alieleza.

Nao baadhi ya Wanafunzi waliopatiwa Elimu juu ya masuala hayo akiwemo Fatma Abdalla Mbarouk  kutoka Skuli ya Msuka Sekondari pamoja na  Ruwaida Salum Hamad  waliwashukuru  Wafadhili hao waliojitolea kuwafikishia Elimu hiyo  ambapo walisema itawasaidia katika kukabiliana na changamoti ambazo walikuwa wanakumbana  nazo awali kabla ya kupata Elimu hiyo. 

 "Tunaahidi kuifanyia kazi Elimu hii ili isiwe kikwazo tena kwetu kupata changamoto zinazopelekea kuwa watoro tunapokuwa katika Hedhi ",Alisema Fatma Abdalla Mbarouk. 



Waliyaomba na Mashirika mengine pamoja na taasisi mbali mbali waige mfano huo mzuri ambao utasaidia kufanikisha malengo ya Wanawake waliyojiwekea kwani bado Elimu hiyi na Taulo hizo  wapo wanafunzi wengi ambao wanazihitaji katika skuli nyengine . 

Elimu iliyotolewa kwa wanafunzi hao ni pamoja na  namna ya kujikinga na kutambua viashiria vya Ukatili wa kijinsia, matumizi salama ya Taulo za kike za kufua, pamoja na haki ya Kisheria ya Afya ya Hedhi Salama kwa Wanafunzi wa kike Maskulini ikiwa ni shamra shamra za  kuelekea siku ya Wanawake Duniani ambapo ugawaji wa Taulo hizo  zimepatikana kupitia kupitia Kampeni ya Twende pamoja  Run for Binti  Marathon. 


                             .MWISHO.

Comments

Popular posts from this blog

AFISI YA MWANASHERIA MKUU ZANZIBAR YAKUSANYA MAONI SHERIA YA MSAADA WA KISHERIA

MKURUGENZI HANIFA, AWAUMA SIKIO WANANCHI WAWI HAKI ZA BINAADAMU

‘WANANCHI HAWANA MAMLAKA YA KUONDOSHA UHAI WA MTU’