..........FUATILIENI MABADILIKO YA SHERIA MSIJEWAPOTOSHA WANANCHI

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WASAIDIZI wa sheria nchini, wameshauriwa kuwa wafuatiliaji na kujisomea zaidi, ili kujua mabadiliko ya sheria, ili kuwarahisishia wanapokwenda kwa wananchi kutoa elimu.

Ushauri huo umetolewa Machi 30, 2023 na Afisa wa Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria Zanzibar Ali Haji Hassan, wakati akiwasilisha mabadiliko ya sheria, ikiwemo ya Ushahidi nambari 9 ya mwaka 2016, kwenye mafunzo kwa njia ya zoom kwa wasaidizi wa sheria.

Alisema, moja ya jukumu la msaidizi wa sheria ni kufuatilia kwenye mamla husika, ili kujua ikiwa kuna mabadiliko ya aina yoyote, ili yamsaidie katika utoaji wake wa elimu kwa jamii.

‘’Sisi wasaidizi wa sheria na wengine, tuweni makini kila wakati ili kutambua ikiwa kuna mabadiliko ya sheria au matamko mengine, ili tuwalishe wananchi chakula halali,’’alisisitiza.

Akizungumzia mabadiliko ya sheria ya ushahidi iliyokuwa ya mwaka 1917 na kupatikana kwa sheria nambari 9 ya mwaka 2016, alisema imekuja kuweka mazingira mazuri kwa mashahidi.

‘’Sheria hii sasa imekuja kuweka ulinzi maalum kwa mashahidi, lakini pia imekuja kuutambua ushahidi wa mtoto, ushahidi wa kielektroniki ukiwemo wa picha na sauti,’’alielza.

Kuhusu mabadiliko ya sheria Mahakama ya Ardhi nambari 7 ya mwaka 1994 kama ilivyorekebishwa kuwa nambari 1 ya mwaka 2008, alisema imekuja kuondosha baadhi ya changamoto.

‘Moja ambalo limekuja ndani ya sheria hii ni Mwenyekiti wa mahakama hiyo, sasa rais kaba ya kumteua sheria imemlazimisha, ashauriane na Jaji Mkuu,’’alieleza.

Aidha alisema jengine lilomo kwenye sheria hiyo mpya ni Mwenyekiti huyo kutambuliwa kwa saifa ya shahada ya kwanaza ya sheria.

Kwa upande wake Afisa sheria kutoka Idara hiyo Salma Suleiman, akiwasilisha mabadiliko ya sheria ya watu wenye ulemavu ya nambari 8 ya mwaka 2022, alisema imekuja kuelekeza makosa mbali mbali.

‘’Kwa mfano yametajwa makosa ya kumuigizia kwa sauti, mwendo, kumdharau, kumkebehi, kumfungia ndani na kumbagua, ambapo baadhi yao hayakuwemo kwenye sheria kongwe ya nambari 9 ya mwaka 2006,’’alieleza.

Aidha Afisa huyo alieleza kuwa, ni wakati sasa kwa wasaidizi wa sheria kuchukua juhudi za maksudi za kuzitambua sheria kongwe na mpya, ili iwe rahisi wanapotoa elimu kwa jamii.

Afisa kutoka taasisi ya LSF Alphonce Marandu, alisema wasaidizi wa sheria wamekuwa kimbilio kubwa kwa jamii, hivyo lazima wajiendeleze.

Khamis Faki kutoka Jumuia ya wasaidizi wa sheria Wete, alisema elimu zaidi inahitaji kila siku kwa jamii, katika kushirikiana na wasiaidizi wa sheria.

Akizungumza nje ya mkutano huo, Mkurugenzi wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’ Nasor Bilali Ali, alisema jambo linalofanywa na LSF na Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria, ni jema.



‘’Mafunzo ya kukumbushwa sheria mpya zilizofanyiwa marekebisho na nyingine kufutwa ni jambo jema, maan sisi wasaidizi wa sheria ndio ambao tunakwenda kwa jamii kila siku,’’alifafanua.

Mafunzo ni muendelezo wa ushirikiano kati ya LSF na Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar, katika kuwaendeleza na kuwaongezea maarifa wasaidizi wa sheria.

                   Mwisho   

     

Comments

Popular posts from this blog

AFISI YA MWANASHERIA MKUU ZANZIBAR YAKUSANYA MAONI SHERIA YA MSAADA WA KISHERIA

MKURUGENZI HANIFA, AWAUMA SIKIO WANANCHI WAWI HAKI ZA BINAADAMU

‘WANANCHI HAWANA MAMLAKA YA KUONDOSHA UHAI WA MTU’