MSAIDIZI WA SHERIA WAWI, AKAGUZWA ARDHI INAYODAIWA KUVAMIWA NA SERIKALI
NA MWANDISHI WETU, CHAPO@@@@
MKURUGENZI wa Jumuiya ya Wasaidizi wa
sheria wilaya ya Chake chake Nassor Bilali Ali, amewataka wamiliki wa ardhi
wanaoishi mbali nazo, kujenga utamaduni wa kuzikagua kila, wakati, ili
kuepushwa kuvamiwa.
Mkurugenzi
huyo aliyasema hayo Machi 24, 2023, eneo Kwasharifuali shehia ya Wawi, wakati
akizungumza na walalamikaji wa eneo hilo, walilodai kuvamiwa na Kiwanda cha mafuta
ya makonyo zaidi ya miaka sita sasa, kwa shughuli za upandaji wa miti ya
biashara.
Alisema,
ardhi iliyokaa bila ya kuendelezwa na kisha mmiliki kushindwa kuipitia kila
wakati, huwa rahisi mtu yeyote kuanzisha matumizi.
Alieleza
kuwa, kama mmiliki anaishi mbali na ardhi husika, ni vyema wakaanzisha uwakala
wa ulinzi wa ardhi zao, ili iwe rahisi kupatikana taarifa kwa aina yoyote ile
ya matumizi.
Mkurugenzi
huyo wa CHAPO alisema, wamekuwa wakijitahidi kutoa elimu kwa wananchi mbali
mbali, juu ya umuhimu wa matumizi ya ardhi.
‘’Wananachi
tunawashauri kama wana ardhi ambazo hawajakuwa tayari kuzitumia wao, basi
wawape watu wengine kwa maandishi ya mkataba maalum, ili kuepusha wengine
kuivamia,’’alieleza.
Katika eneo
jingine, alisema ardhi sasa imekugeuka dhahabu kwa kila mmoja, hivyo ni wajibu
wa kila mmiliki, kuhakikisha anairasimishi.
‘’Ardhi
iliyopimwa, inakuwa na thamani mara mbili, na inaweza kutumika kama kizibiti
cha kuombea mkopo katika taasisi mbali mbali za fedha,’’alifafanua.
Akizungumza kwenye ukaguzi huo, Msaidizi wa sheria Jimbo la Wawi Haji Nassor Mohamed, alisema baada ya kupokea malalamiko ya familia Machi 22, 2023, juu ya madai ya kuvamiwa ardhi yao, alifika kwa walalamikiwa.
Alisema kisha Machi 23, 2023 alifika kwa Uongozi wa Kiwanda cha Mafuta ya Makonyo Wawi, pamoja na uongozi wa shehia ya Wawi, juu ya kuwasilisha lalamiko husika.
Kisha uongozi wa Kiwanda cha Mafuta ya Makonyo, ilipofika Machi 24, ulipenda kukutanishwa na familia inayodai kuvamiwa eneo lao, na baada ya ukaguzi, mazungumzo ya awali yalifanyika.
''Mazungumzo ya awali baina pande mbili hizo, mbele ya Msaidizi wa sheria na sheha wa shehia ya Wawi yalifanyika, ingawa baada ya Kiwanda kudai kuwa wamekodishwa ardhi hiyo, familia inafuatilia Wizara ya Kilimo,''alieleza.
Hata hivyo Msaidizi huyo wa sheria, alisema tokea aanze kazi shehiani humo mwanzoni mwa mwaka huu, migogoro ya ardhi inaonekana kuchukua nafasi, kwani tayari ameshasaidia kufikia mwafaka kwa mgororo wa kuwania mpaka.
Sheha wa
shehia ya Wawi Sharifa Waziri Abdalla, alisema alipokea malalamiko hayo, Machi
22, 2023 kwa familia ya Ali Hamad Kheir, ikilalamikia ardhi yao kuvamiwa.
Alisema
alifikisha malalamiko hayo kwa uongozi wa Kiwanda cha mafuta ya makonyo Wawi,
na kutaka kukutana na wanafamilia, wanaolalamika.
Alisema,
amekuwa akipokea migogoro kadhaa ya ardhi, ingawa hatua ya kwanza ni
kuzikutanisha pande mbili hizo, na kisha kuangalia, ikiwa sulhu imepatikana.
‘’Kwa sheria
zilivyo, wao wenyewe kwanza hutakiwa kufanya mazungumzo ya awali, ikiwa hakuna
shida wanaweza kumaliziana,’’alieleza.
Ali Salim
Rashid, akizungumza kwa niaba ya familia yake, alisema eneo hilo hadi mwaka
2017, lilikuwa halijavamiwa kuwa kupandwa aina yoyote ya miti.
‘’Lakini
kuanzia mwaka 2018, tuliona mmeshapandwa michai chai na mikaratusi,
tulipofuatilia tuliambiwa ni mali ya Kiwanda cha mafuta ya makonyo Wawi, na
tulianza kufuatilia hapo zamani,’’anasema.
Uongozi wa
Kiwanda hicho, ulisema eneo hilo walilipata kutoka mikononi mwa wizara ya
Kilimo, na wanalikodi kuanzia mwaka 2001 hadi sasa.
‘’Sisi ardhi
hii tumekodishwa na wizara ya Kilimo, tokea mwaka 2001, na tunalipa kila mwaka,
hivyo sisi hatujui ilipopatikana, inabidi familia inyolalamika, iende mbele
zaidi,’’ulisema uongozi wa Kiwanda.
Kiwanda cha
mafuta ya makonyo Wawi, katika eneo la Mtakata lina wastani wa ekari 550, kwa
ajili ya shughuli za kilimo cha mchai chai na mikaratusi kwa ajili ya
uzalishaji mafuta.
Mwisho




.jpg)





Comments
Post a Comment