SHEHIA YA MVUMONI WAZINDUA KAMATI YA KUPINGA UDHALILISHAJI

 

NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@


MKUU wa Idara ya Wazee na Ustawi wa Jamii Pemba, Omar Mohamed Ali amesema kuwa kuundwa kwa kamati ya kupinga na kupambana na vitendo vya udhalilishaji, itasaidia kwa kiasi kikubwa, kuandaa jamii yenye ustawi bora ambayo itawaweka wanawake na watoto, katika mazingira yaliyosalama.

Alisema kuwa vitendo vya ukatili na udhalilishaji kwa wanawake na watoto, bado vinaendelela kujitokeza katika jami, hivyo serikali, inaendelea kutumia mbinu tofauti, ikiwemo kuunda kamati za shehia, wilaya, mkoa na taifa, ili kupambana na na vitendo hivyo.



Aliyasema hayo katika uzinduzi wa kamati ya kupinga udhalilishaji dhidi ya wanawake na watoto shehia ya Mvumoni, hafla iliyofanyika skuli ya sekondari ya Furaha.

Alieleza kuwa, kuwepo kwa vitendo hivyo vimekuwa vikiwarudisha nyuma, baadhi ya jamii kwa kuona muhali wa kuviripoti, hivyo uwepo wa kamati hiyo inaweza kuwa mwarubaini.

 
"Nendeni mkafanye kazi kwa kuielimisha jamii, juu ya athari ya vitendo vya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia pamoja na kuondosha muhali wa kuvinyamzia kimya, ili kupata ustawi ulio bora na kuwaweka wanawake na watoto, katika mazingiara yaliyosalama.

Mkuu huyo ameitaka kamati hiyo kutokatishwa tamaa na baadhi ya watu, kwenda kutetea maslahi ya wanwake na watoto katika shehia hiyo.

Mapema mjumbe wa kamati ya kupambana na udhalilishaji wilaya ya Chake chake Burhani Khamis Juma, alisema kuwa udhalilishaji unajumuishwa siyo tu vitendo vinavyopelekea madhara ya kimwi, bali hata mateso na kudharauliwa.


Alisema kuwa matokeo ya udhalilishaji ni makubwa yanayoweza kusababisha majaraha, kifo, kisaikolojia, tabia hataraishi na matokeo mabaya ya kielimu na kikazi.


"Mnawajibu mkubwa wa kuzuia, kupinga na kupambana udhalilishaji, na kuna kila aina ya kuwasaidia watoto na kueleza athari za vitendo hivyo, ili kusaidia jamii na serikali kiujumla,"alifafanua.


Kaimu sheha wa Mvumoni Fatma Ali  Khamis alisema kuwa, kuundwa kwa kamati hiyo itahakikisha inaweka mikakati ya mizuri ya kuwasaidia wananchi wake, ili kuonesha mfano kwa shehia nyingine juu vitendo hivyo.


Msaidizi wa sheria shehia ya Mvumoni Haji Nassor Mohamed, alisema kuwa lengo la kuwepo kamati hizo ni kupinga na kupambana na udhalilishaji, ili kuwaweka salama wanawake na watoto.

"Tumeunda kamati ya kupinga na kupambana na vitendo vya udhalilishaji, ili kwenda kuisaidia jamiii kwa kuwapa elimu hiyo, na kuhakikisha wanawake na watoto wanabaki kuwa salama, wasifanyiwe udhalilishaji,"alifafanua.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Jumuiya ya Wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Fatma Hilali Salu, alisema kuwa, Jumuiya hiyo ipo kisheria chini ya ofisi ya Katiba na sheria, kwa lengo la kutoa msaada wa kisheria bila ya malipo kwa wananchi.



Alisema kuwa Jumuiya ipo kwa kuwasaidia wananchi wa tabaka la chini wasiyo na kipato ili kupata haki zao kwa wakati.
 



Nae Mratibu wa kamati hiyo Hawa Kassim Omar, alisema anafarajika kuzinduliwa kwa kamati hiyo, kwani alikuwa akifanyakazi katika mazingira magumu.



Kamati hiyo imeundwa  kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, ikiwemo sheha, Naibu sheha, diwani, mratibu wa shehia, msaidizi wa sheria, waalimu wa wakuu, washauri nasaha na kundi la watu wenye ulemavu.


MWISHO.

 

Comments

Popular posts from this blog

AFISI YA MWANASHERIA MKUU ZANZIBAR YAKUSANYA MAONI SHERIA YA MSAADA WA KISHERIA

WAJUMBE SHEHIA MVUMONI WAPIGWA MSASA ELIMU YA KISHERIA

BODI CHAPO YANG'AKA UTORO, UVIVU WA WASAIDIZI WA SHERIA