WAZO LA MSAIDIZI WA SHERIA LAKUBALIWA MVUMONI
NA AISHA MOHAMED, PEMBA@@@@
MSAIDIZI wa sheria
shehia ya Mvumoni wilaya ya Chake Chake Pembaa, Haji Nassor Mohamed, ameutaka
uongozi wa shehia hiyo, kuifufua kamati ya kupambana na vitendo vya
udhalilishaji, ili vitendo hivyo visiendelee kuwathiri wanawake na watoto.
Msaidizi huyo wa
sheria, aliyasema hayo jana kituo cha afya Mvumoni, kwenye mkutano maalum unaolenga,
kuifufua kamati hiyo, na kuhudhuriwa na wajumbe wa sheha na mratibu wa wanawake
na watoto wa shehia hiyo.
Alisema lengo la kikao hicho ni kuja kuifufua kamati
ya kupambana na vitendo vya udhalilishaji, ambayo ilionekana kusizi, ili kuweza
kuvipunguza vitendo hivyo shehiani humo.
Alisema vitendo
vya udhalilishaji vipo katika shehia za wilaya ya Chake chake ikiwemo ya Mvumoni,
hivyo ni wakati sasa kuifufua na wajumbe wake wake, kufanyakazi wa bidi.
“Nawaomba sana
wajumbe wa kamati na sheha mwenyewe, tushirikiane na mratibu wetu wa wanawake
na watoto wa shehia, ili kuona sasa kamati hii, inafanyakazi zake,’’alifafanua.
Kwa upande wa
Katibu wa Kamati ya kupambana na udhalilishaji wilaya ya Chakechake Rashid Said
Nassor aliahidi kushirikiana na kamati hiyo, ili kuhakikisha vitendo hivyo
haiendelei kawatesa wanawake na watoto.
Aidha aliahidi kuwapa
elimu, mara tua atakapoarifiwa juu ya kuundwa na kuanza kazi kwa kamati hiyo ya
shehia ya Mvumoni wilaya ya Chakechake.
‘’Katika kuinga
mkono kamati hiyo, naahidi kusaidia vitendea kazi, ikiwemo karatasi na vifaa
vingine, ili kamati ifanye kazi kwa ufanisi,’’alifafanua.
Hata hivyo aliwataka
wananchi wa shehia hiyo, kumtumia kwa karibu Msaidizi wa sheria walie nae, ili
kutatuliwa changamoto zao kadhaa za kisheria.
Akizungumzia muu
wa kamati hiyo, alisema sheha wa anakuwa ndie Mwenyekiti, Mratibu wa wanawake
na watoto Katibu na wajumbe wingine kutoka kila makundi yaliomo ndani ya
shehia.
‘’Msaidizi wa
sheria anakuwa mjumbe, Askari wa shehia, watu maarufu, viongozi wa dini,
waalimu wakuu, mabaraza ya vijana na makundi ya watu wenye ulemavu,’’alifafanua.
Mapema Mratibu wa
wanawake na watoto wa shehia ya Mvumoni Raisa Salim Mohamed, alisema kuwa
kamati ipo ingawa, haina wajumbe, waliomo mwenye muunndo wa kisheria.
‘’Kazi nafanya
kila siku, ingawa nashirikiana na wajumbe wa kamati ya sheha na wakati mwingine
waalimu wa skuli na madrassa, inapohitajika,’’alifafanua.
Hata hivyo,
alisema ipo haja ya kuwepo kwa wajumbe waliotajwa kwenye muongozo, kwani bado
matendo hayo yanaripotiwa kila siku.
Nae Katibu wa
sheha wa Mvumoni, Khamis Mohamed Abdallah, ametoa shukran kwa msaidizi wa
sheria na katibu wa kamati ya kupambana na udhalilisha ya wilaya ya Chakechake,
kwa kuja na wazo hilo.
“Kwakweli
tunashukuru sana msaidizi wa sheria na katibu, maana hili jambo lilikuwa linatuumiza
kichwa, hatujui nini tufanye, ingwa sasa ujio wenu tumeshapata mwanga,’’alifafanua.
Takwimu
zilizokusanywa na Ofisi ya Mtakwimu mkuu wa serikali Zanzibar, iliripoti
matukio 1,809 ya ukatili na udhalilishaji wa kijinsia, kwa mwaka 2024, ambapo waathirika walikuwa 1,809 na wengi walikuwa watoto sawa na
asilimia 84.3.
Wilaya ya Chake
chake, ilishika nafasi ya nne, kwa kuripoti matukio 113,
kati ya wilaya 11 za Unguja na Pemba, huku wilaya ya Magharibi ‘B’ Unguja,
ikiwa ya mwanzo kwa matukio 431.
Kwa mwaka jana,
matukio hayo kwa Unguja na Pemba, yalipungua 581, maana yalikua 1,228, kinyume
na yake 1,809 ya mwaka 2024, jambo hata baadhi ya wilaya, ikiwemo ya Chake
chake, nako yaliripotiwa kushuka.
Wilaya
iliyoongoza kwa mwaka jana ni Magharibi ‘A’ kwa matukio 247, na wilaya ya Chake
chake safari hii, ilipanda nafasi moja, ingawa iliripoti matukio kiduchu 93,
tofauti na matukio 113 ya mwaka 2024.
Waathirika
wakubwa kwa mwaka 2025, ni watoto, waliokuwa 1,050 sawa na asilimia 85.4 kwa
Unguja na Pemba, wakifuatiwa na wanawake 162 asilimia 13.2 na wanaume 18, sawa
na asilimia 1.5.
Mwisho







Comments
Post a Comment