WANACHAPO WAPEWA MAFUNZO AKILI MNEMBA 'AI'
NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@
WANACHAMA
wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’ wamepatiwa
mafunzo ya matumizi ya akili ya kisayansi ‘akili mnemba’, baada ya watendaji wa
wawili wa jumuiya hiyo, kumaliza mafunzo kama hayo, wiki iliyopita.
Kabla ya
kuanza kwa mafunzo hayo, Mkurugenzi wa ‘CHAPO’ Mohamed Hassan Abdalla, alisema
utaratibu kwa sasa utakuwa kwa kila atakayerudi kwenye mafunzo, kuhakikisha
anawapa na wenzake.
Alisema,
mpango huo ulikuwepo zamani, ingawa katika siku za hivi karibuni, ulionekana
kufa, na wakati umefika sasa kuufufua, ili kuona nguvu zinazotumiwa na
washirika wao, zinaungwa mkono.
Akitoa mada
ya mafunzo hayo ofisini kwao Chake chake jan August 17, 2025, alisema akili mnemba, ni mfumo wa kompyuta
ambao umeshajazwa taarifa kadhaa, ambazo ni za ukweli, kwa ajili ya matumizi.
‘’Raha ya tovuti
hii, unaweza kuiuliza taarifa ambazo zimeshachaktwa, na tayari kwa ajili ya
matumizi ndani ya jamii,’’alisema.
Akizungumzia
faida ya mifumo hiyo hasa kwa wasaidizi wa sheria katika kazi zao za kila siku,
alisema ni pamoja na kujirahisishia wakati wanapoandaa mada.
Alifafanua kuwa,
moja ya jukumu la wasaidizi wa sheria ni kuifikia jamii, na kutoa elimu iwe ya
ardhi salama, mirathi, udhalilishaji, vyeti vya kuzaliwa na makundi ya watu
maalum.
‘’Haya yote,
kama huyajui kama yalivyo, unaweza kutumia mfumo huo wa ‘GPT’ na ukiomba
unaweza kupata majibu halisi na kuyatumia ndani ya kazi zenu,’’alifafanua.
Mapema Mkurugenzi
huyo, aliwapokea wasaidizi wapya wa sheria watano, ambao walimaliza mafunzo yao
hivi karibuni, wakitokea shehia za Ng’ambwa, Mfikiwa, Ndagoni, Ziwani na Mjini
Ole.
Hata hivyo
aliwataka wasaidizi wa sheria wakongwe, kuwapa kila aina ya ushirikiano wenzao
wapya, ili kuwafikia wananchi kuwapa elimu, ushauri na msaada wa kisheria.
Mapema Mkurugenzi
fedha wa ‘CHAPO’ Riziki Hamad Ali, aliwakumbusha wasaidizi hao wa sheria, kuharakisha
kuwasilisha ripoti kazi za utendaji wa kila mwezi.
Alisema wapo
baadhi, wamekuwa hawawasilishi kazi zao kwa wakati, na kusababisha usumbufu
wakati wa kuandika ripoti ya pamoja ya jumuiya.
Wakati huo
huo, aliwapitisha kwenye fomu ya utoaji wa elimu na msaada wa kisheria, na
kuwataka ikiwa watakwama, kuwasiliana na wenzao wakongwe kwa maelekezo.
Mapema wanachama wa CHAPO, walilipitisha jina la Fatma Hilali Salum, kushika nafasi ya Mratibu wa CHAPO, kuanzia August 17, ya mwaka huu.
Mara baada
ya kupokea nafasi hiyo, aliomba ushirikiano wa karibu na watendaji wa CHAPO, ili
kufikia malengo ya jumuiya yao.
Baadhi ya
wasaidizi wa sheria akiwemo Jafari Abdalla Ali wa shehia ya Mgogoni na Abass Maalim
Abeid wa Pujini, wamewahimiza wenzao, kuongeza juhudi za kuwafikia wananchi kuwapa
elimu.
Hata hivyo, walipongeza
kupatiwa mafunzo ya akili bandia, na kusema yatawasaidia kwa kiasi kikubwa,
katika kazi zao kila siku, na hasa kuandika hati za madai.
Nae msaidizi
wa sheria Saada Hamad Mbarouk wa Ole, alisema kuanzia sasa, atautumia mfumo huo
wa kompyuta wa akili bandia, wakati anapotaka kuandaa mada zake.
CHAPO,
imekuwa na utaratibu kila mwezi mara moja kukutana na watendaji wake, na
kuelezeana mafanikio na changamoto za mwezi uliokwisha.
Mwisho







Comments
Post a Comment