CHAPO: WASAIDIZI WAPYA WA SHERIA MASHEHA NDIO WENYEJI WENU SHEHIANI

 




NA HAJI NASSOR, PEMBA::


WASAIDIZI wapya wa sheria wa majimbo ya wilaya ya Chake chake kisiwani Pemba, wametakiwa kushirikiana na masheha kwenye shehia zao, ikiwa wanata kufanikiwa katika kazi zao, za utoaji elimu, msaada na ushauri wa kisheria kwa wananchi.

Kauli hiyo imetolewa leo Januari 27, 2023 na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’ Safia Saleh Sultan, wakati akizungumza na wasaidizi hao, ofisini hapo mjini Chake chake.

Alisema, kila msaidizi wa sheria, mwenzake katika shehia yoyote ile ni Sheha wa shehia husika, kwani ndie mwenyeji wake kikazi, na si vyema kumdharau.

Alieleza kuwa, kazi ya msaidizi wa sheria moja ya wajibu wake, ni kuhakikisha anafanyakazi bega kwa bega na sheha au wajumbe wa sheha, ili kufanikisha kazi zao zake.





‘’Mnakwenda kwenye shehia, lakini muelewe kuwa, msishahu kuwa Sheha ndio mwenyeji wako, na usijaribu kufanya jambo lolote, pasi na kumuomba ruhusa,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, Mwenyekiti huyo wa Bodi ya CHAPO, alifahamisha kuwa, ushirikiano baina ya wasaidizi hao wa sheria wapya na wale wakongwe, ni jambo la muhimu.

‘’Sote tunajenga nyumba moja ya kuisaisdia jamii yetu, sasa hakuna huja ya mivutano, bali ili mufanikiwe mujenge ushirikiano,’’alieleza.

Hata hivyo ameutaka uongozi wa CHAPO, kuendelea kukutana na wasaidizi hao wa sheria kila wakati, hasa kipindi hiki wakiwa bado wachanga katika kazi hiyo.

Kwa upande Mkurugenzi wa ‘CHAPO’ Nassor Bilali Ali, alisema kwa vile wasaidizi hao wapya wa sheria wameshajisajili na kutambulika, kazi iliyoko mbele yao sasa ni kuihudumia jamii.

Aliongeza kuwa, moja ya majukumu ya msaidizi wa sheria ni kutoa elimu, ushauri na msaada wa kisheria kwa watu wasio na uwezo, tena bila ya malipo.

‘’Mukumbuke kuwa, moja ya kazi zenu ni kutoa elimu, na msaada wa kisheria tena bila ya malipo, maana kazi hii, zaidi msingi wake ni kujitolea,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, Mkurugenzi huyo wa CHAPO, alisisitiza haja kwa wasaidizi hao wa sheria, kuendelea kujifunza kwa kusoma machapisho mbali mbali ya kisheria.




Msaisdizi wa sheria jimbo la Chonga Juma Seif Haji, alisema atahakikisha anashirikiana na sheha na wasaidizi wa sheria waliomtangulia, ili kufanikisha azma ya kuwahudhumia wananchi.

Nae msaidizi wa sheria Jimbo la Chake chake, Wahida Kombo Khamis alisema kazi hiyo inahitaji umakini mkubwa, ili kuhakikisha jamii haiyumbi.

Wasaidizi hao wa sheria wapya, tayari wameshakamilisha usajili chini ya Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria pamoja na kujiunga na Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake Chake ‘CHAPO’.

                     Mwisho   

Comments

Popular posts from this blog

AFISI YA MWANASHERIA MKUU ZANZIBAR YAKUSANYA MAONI SHERIA YA MSAADA WA KISHERIA

MKURUGENZI HANIFA, AWAUMA SIKIO WANANCHI WAWI HAKI ZA BINAADAMU

‘WANANCHI HAWANA MAMLAKA YA KUONDOSHA UHAI WA MTU’