MDHAMINI KATIBA, SHERIA: 'AWAPA TANO WASAIDIZI WA SHERIA PEMBA'
NA
HAJI NASSOR, PEMBA::
AFISA
Mdhamini wizara ya nchi afisi ya rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora
Pemba Halima Khamis Ali, amesema kazi inayofanywa na wasaidizi wa sheria na
watoa msaada wa kisheria, imesaidia kuonesha jamii njia ya haki na kuacha
batili.
Afisa Mdhamini huyo aliyaeleza hayo, ukumbi wa wizara
hiyo, kwenye mkutano wa robo mwaka, wa masuala ya msaada wa kisheria,
ulioandaliwa na Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria Zanzibar.
Alisema, licha ya changamoto kadhaa walizonazo watoa na
wasaidizi hao wa msaada wa kisheria hao, lakini kwa sasa hali inaridhisha ya
wananchi, kuzijua haki zao mbali mbali.
Alieleza kuwa, jamii awali haikuwa na uwelewa mpana wa
haki zao mbali mbali, lakini baada ya Idara ya Katiba na Msaada wa sheria
kuwajengea uwezo na kisha kwenda mtaani, hali inaridhisha.
‘’Kwa haki bado msingi mkuu kwa jamii kuzipata na kuzijua
haki zao zitabakia kuwa, zimeimarisha na watoa na wasaidizi wa sheria waliomo
shehiani, kwa hili hongereni,’’alifafanua.
Katika hatua nyingine, Afisa Mdhamini huyo, amewataka
wasaidizi hao wa sheria, kuyafanyiakazi maazimio wanayokubaliana, katika vikao kama
hivyo.
‘’Moja ya jambo ambalo kwenye mkutano wa mwaka jana
mlilipitisha ni nyinyi kupata mafunzo ya upigaji picha, mafunzo ya lugha za
alama, lakini mmeshindwa kufanikisha kwa sababu nyepesi,’’alieleza.
Mapema akizungumza kwenye mkutano huo, Afisa sheria
kutoka Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria Zanzibar Ali Haji Hassan, alisema
bado jitihada zinahitajika kwa wasaidizi wa sheria, katika kuifikia jamii.
Hata hivyo amewakumbusha watoa msaada hao na viongozi wa jumuiya
ya wasaidizi wa sheria, kuwakumbusha wanachama wao kujisajili, kwani kinyume
chake, kisheria hawezi kuihudumia jamii.
‘’Sheria yetu inatuongoza kuwa, kila mwaka tufanya
usajili na hili ni takwa la kisheria, na kinyume chake Idara na hata hizo
Jumuiya itakuwa hazitambui uwepo wenu,’’alieleza.
Akiwasilisha tathmini ya jukwaa la pili la mwaka la
msaada wa kisheria Zanzibar, Afisa huyo alisema mengi yamejitokeza, ikiwa ni
pamoja na wazo la kuundwa mfuko wa wasaidizi wa sheria.
Alisema, jengine ni kuendelea kujengewa uwezo wasaidizi
wa sheria, ili kuwa wabunifu katika utendaji wao wa kazi, ili kutimiza malengo
yao.
Akiwasilisha ripoti ya utendaji, Mkurugenzi wa Jumuia ya
wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba, ‘CHAPO’ Nassor Bilali Ali,
alisema wamekuwa wakishirikiana na taasisi mbali mbali, katika kuwafikia
wananchi.
‘’Tumekuwa tukishirikiana na Kituo cha Huduma za Sheria
Zanzibar ‘ZLSC’, TAMWA-Zanzibar, TUJIPE, na jumuiya nyingine za wasaidizi wa
sheria kisiwani Pemba,’’alieleza.
Nae Mkurugenzi wa wasaidizi wa sheria wilaya ya Mkoani ‘MDIPAU’
Nassor Hakim Haji, alisema changamoto kubwa wanayoiona na jamii, kutokuwa
tayari kuhudhuria kwenye vikao vyao.
Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar, imekuwa
ikiendesha mafunzo, makongamano na majukwaa kwa wasaidizi wa sheria na watoa
msaada wa kisheria, ili kuwajengea uwezo katika kazi zao.
Mwisho








Comments
Post a Comment