'WALINDENI WATOTO NA WATUMIAJI WA DAWA ZA KULEVYA'

 

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANANCHI wa kijiji cha Birikau shehia ya Michungwani wilaya ya Chake chake Pemba, wametakiwa kuwalinda watoto wao, kwani watumiaji, wasafirishaji na waingizaji wa dawa za kulevya, wamekuwa wakiwatumia watoto, katika kufanikisha malengo yao.

Ushauri huo umetolewa April 30, 2024 na Askari kutoka Jeshi la Polisi wilaya ya Chake chake, anayezifanyia kazi shehia za Wesha, Michungwani na Ndagoni wilayani humo Khamis Ali Khamis, wakati akizungumza na wananchi, kwenye mkutano wa wazi.

Alisema, kwa sasa watumiaji na wasafirishaji wamekuwa wakiwatumia watoto, wakijua kuwa, kisheria hawashatakiwa na wakati mwingine hawawezi kupekuliwa.



Alieleza kuwa, taarifa zipo zinazoenesha kuwa, sasa watoto wamekuwa wakitumiwa na watumiaji, wasaambazaji wa dawa za kulevya, baada ya mitego ya kuwatumia watu wazima kugundulika.

‘’Wazazi wa kijiji ch Birikau, kuweni makini mno na wasambaazaji, watumiaji, wauzaji na waingizaji wa dawa za kulevya, sasa wamehamishia kazi hiyo kwa watoto,’’alieleza.

Katika hatua nyingine Askari huyo wa shehia, aliwataka wazazi na walezi hao, kufufua malezi ya pamoja miongoni mwao, ambapo kufanya hivyo wanaweza kuwakinga na majanga watoto wao.

‘’Leo kila mmoja ni shahidi kuwa, watoto wamekuwa na ugumu kwenye malezi, sasa tusiporejesha malezi yale ya zamani, ya kuhakikisha tunaleleana watoto, majanga yanaweza kuwa mingi kwao,’’alieleza.

Katika hatua nyingine Askari huyo, aliwataka wananchi hao kutoa taarifa wakati wowote katika vyombo husika, wanapoona viashiria vya vijana wanaotaka kutumia dawa za kulevya.

Mapema Msadizi wa sheria wa shehia za Wesha, Michungwani na Ndagoni Khadija Said Khalfan, aliwakumbusha wazazi na walezi hao, kukaa na watoto wao kila wakati, ili kuwagundua ikiwa wameanza kudhalilishwa ama laa.

Alieleza kuwa, wazazi wasipokuwa karibu na watoto wao, wanaweza kukumbwa na majanga ya udhalilishaji na kuchelewa kuwagundua, ikiwa wameanza kufanyiwa vitendo hivyo.




Wakati huo huo, Msaidizi huyo wa sheria amewataka wananchi kuwatumia wasaidizi wa sheria kutoka Jumuiya ya wasaidizi wa sheria CHAPO, waliomo shehiani mwao, wanapokuwa na changamoto za kisheria.

‘’Njooni kwetu mpate ushauri na msaada wa kisheria bila ya malipo, kwani moja ya jukumu letu ni kuhakikisha wananchi waliopoteza mwelekeo wa kupata haki zao, wanasaidiwa,’’alieleza.

Mmoja wa mzazi wa kijiji hicho, Salama Makame Haji, alisema elimu bado inahitajika kwa jamii, juu ya namna kutoa taarifa wanapoona viashiria vya udhalilishaji.

Nae mwananchi Hamza Salum Khamis, alisema kama sheria inaukubali ushahidi wa picha, katika makosa ya jinai, imekuwa jambo zuri kwao, katika kutokomeza makosa hayo.

Katika hatua nyingine Mwalim wa Almadrassatul Jazzira Islammiya ya Birikau Ali Othman Mohamed, amewakumbusha wazazi na walezi, kuwabidiisha watoto wao, juu ya suala la kuhudhuria madrassa.




Akifungua mkutano huo, Mwalimu wa Almadrassatul Zainabiya sheikh Mohamed Omar Mussa, amesema elimu waliyoipata watahakikisha wanaifanyia kazi, ili jamii ipate mabadiliko.

                                   Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

AFISI YA MWANASHERIA MKUU ZANZIBAR YAKUSANYA MAONI SHERIA YA MSAADA WA KISHERIA

MKURUGENZI HANIFA, AWAUMA SIKIO WANANCHI WAWI HAKI ZA BINAADAMU

‘WANANCHI HAWANA MAMLAKA YA KUONDOSHA UHAI WA MTU’