WATOTO WASAKATA SOKA WESHA WALALAMIKIA KUTENGWA MATUMIZI YA UWANJA

 


 NA MARYAM NASSOR, PEMBA@@@@

BARAZA la watoto wa shehia ya Wesha wilaya ya Chake chake Pemba, wamesema changamoto yao ya kukatazwa matumizi ya uwanja wa mpira wa miguu nyakati za jioni, inawanyima fursa ya kujiendeleza, kimichenzo.

Walisema kuwa, changamoto hiyo inawarudisha nyuma kimichezo, kwani hawapati muda mzuri katika kufanya mazoezi yao.

Hayo, yameelezwa na mjumbe wa kamati hiyo, Saidi Mohamed Ali, kwenye mkutano wa wazi, uliyoandaliwa na Jumuiya ya wasaidizi wa Sheria wilaya ya Chake chake (CHAPO), uliofanyika huko Wesha kwa Sheha.

Alisema, watoto katika kijiji  chao, wana malengo makubwa katika soka, kutokana na kuwa, mpira siku hizi ni ajira na biashara pia.

 Alisema kuwa, vijana wengi siku hizi wamefanikiwa kujipitia ajira kupitia soka, hivyo nao kuendelea kubanwa na timu kubwa wasifanye mazoezi, kwenye uwaja  pekee uliopo Wesha, ni kuanza kuzizima ndoto zao.

‘’Kila mmoja asubuhi anakwenda kwenye harakati, sasa jioni ndio wakati wa mazoezi, lakini inapokuja timu kubwa, ambayo chanzo ni sisi wadogo, hutukufukuza,’’alieleza.

“Mpira siku hizi ni ajira, na Serikali yetu, ina malengo makubwa na vijana, katika kutuendeleza kisoka, lakini sisi tunanyimwa hiyo fursa na timu kubwa, katika uwanja wetu,’’alilalamika.

Nae, Samir Magesi alisema  anatamani siku moja kuwa mchezaji wa timu kubwa kama Simba na Yanga, ingawa changamoto ya kuzuiwa kutumia uwanya wa mpira wa miguu, wakati wa jionii  inawarejesha nyuma.



Alisema kuwa, soka la Zanzibar na Tanzania kwa ujumla limekuwa, lakini vijijini bado hakuna viwanja kwa watoto, vya kufanyia mazoezi, ili kujijenga kimichezo.

“Huku kwetu, vijijini watoto hatuna viwanja vya kufanyia mazoezi, ndio maana tunavizia kiwanja cha wakubwa, na sisi kufanya mazoezi, ingawa wenyewe ni wakali,” alisema.





Aidha, aliiomba Serikali ya Mapinduziya Zanzibar kuwajengea viwanya vizuri na watoto wa vijijini ili kukuza vipaji vyao.

Nae msaidizi wa sheria kutoka Shehia ya Wawi, Haji Nassor Mohamed aliwaahidi kuifanyia kazi changamoto yao hiyo, ikiwa na pamoja na kuwaahidi vifaa vya michezo.

Aliwataka, wasikate tamaa, kutokanana changamoto inayowakabili, katika kujiendeleza kimichezo na kufanya bidii ili kufikia malengo yao kimichezo.

                        MWISHO

 

 

 

 

Comments

Popular posts from this blog

AFISI YA MWANASHERIA MKUU ZANZIBAR YAKUSANYA MAONI SHERIA YA MSAADA WA KISHERIA

MKURUGENZI HANIFA, AWAUMA SIKIO WANANCHI WAWI HAKI ZA BINAADAMU

‘WANANCHI HAWANA MAMLAKA YA KUONDOSHA UHAI WA MTU’