CHAPO YAWAONESHA NJIA WANA WAWI KUEPUKA MIGOGORO YA ARDHI
NA ASHA ABDALLA, PEMBA
WANANCHI wa
shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake, wametakiwa kutafuta hatimiliki kutoka
serekalini, maratu baada ya kununua kiwanja, shamba au kipande cha aina yoyote cha ardhi, ili
kuepukana na migogoro isiyokuwa ya lazima.
Hayo yameelezwa Oktoba 28, 2023 na Mjumbe wa Bodi kutoka Jumuiya ya Wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba, ‘CHAPO’ Asha
Sleiman Said, wakati akizungumza na wananchi hao, kwenye mkutano wa wazi
ulioandaliwa na jumuiya hiyo na kufanyika Kunguni Wawi.
Alisema kua, zipo
njia mbali mbali zinazotumiwa ili mtu aweze kupata haki ya kutumia ardhi
bila ya migogoro yoyote, ikiwemo njia yakununua na kupewa hati ya matumizi.
Mjumbe huyo kutoma
CHAPO, alifahamisha kuwa, mwarubaini pekee mara baada ya mtu kununua, kupewa
hiba, kurithi, kuiomba serikalini ni kufuatia hati za umiliki serikalini.
"Kuna maeneo
mbali mbali ambayo tumefanya zoezi la kutoa hati za umiliki wa ardhi, kupitia zoezi
la la utambuzi na usajili wa ardhi, lakini hata baada ya hati kukamilika, watu
hawazichukui,’’alieleza.
Nae Msaidizi wa sheria
sheia ya Wawi Haji Nassor Mohamed, alisema wasaidizi washeria wana nafasi
kubwa katika suala zima la kuelimisha jamii juu ya umuhimu wa kuzilinda haki za
binaadamu.
Alisema kua haki
moja na muhimu ya binaadamu ni ile ya kuishi, ambayo hakuna mwenye mamlaka ya
mwengine kumuondolea mtu haki hiyo.
‘’Ndio maana hapa
tunapinga vikali suala la watu kujichukulia sheria mikononi kwa muua mtuhumiwa
wa wizi wa ndizi, kuku na Ng’ombe kwa madai ya vyombo vya sheria kutokuchukua
hatua,’’alieleza.
Akizungumzia haki ya kupata Habari, aliwataka
wananchi hao wasidharau mikutano hiyo, na waposi”ia upatu ama njia nyingine
yeyote ya taarifa kufika haraka kwenye mikutano inayoitishwa.
Kwa upande wake
Askari shehia kutoka kituo cha Polisi Madungu Chake chake, Issa Ahmada Iddi,
alisema kua, wananchi wanapopatwa na matukio mbali mbali, waepuke
kujichukulia sheria mikononi mwao, kwani vyombo vya ulinzi vipo.
Hata hivyo aliwakumbusha wananchi hao, kufufua
ulinzi ushirikishi, ambao kwa baadhi ya shehia kama vile Mkoroshoni wamefanikiwa
kudhibiti matendo ya uhalifu.
Mwananchi wa shehiya
hiyo Omar Juma Khamis alitoa ushauri kwa serekali, wanapokwenda kupima
ardhi ambayo wanataka kutoa hatimiliki, wapime sehemu zote nne na wahusika wawepo
kushuhudia.
Sheha washehiya
hiyo Sharifa Waziri Abdalla, alisema kua watajitahidi kuchukua taaluma hiyo
walioipata, na kuwapa wenzao, ili kuondokana na changamoto zinazojitokeza za
migogoro ya ardhi na uvunjifu wa haki za binadamu.
Msaidizi wa sheria
shehia ya Wawi na Mgogoni Fatma Hilali Salim, alisema wanaendelea kutoa
ushauri, elimu na msaada wa sheria bila ya malipo kwa wanancho wote.
MWISHO









Comments
Post a Comment