WASAIDIZI WA SHERIA 'CHAPO' WAKUMBUSHWA JAMBO MUHIMU
NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@
WASAIDIZI wa sheria wilaya ya Chake
chake Pemba, wakumbushwa kuwahudumia wananchi kwa kuwapa elimu, ushauri na
msaada wa sheria, ili iwe rahisi kupata ufumbuzi wa haki zao.
Ushauri huo
umetolewa leo Mei 7, 2023 na Mkurugenzi wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake
Pemba ‘CHAPO’ Nassor Bilali Ali, wakati akizungumza na wasaidizi hao wa sheria,
kwenye kikao maalum cha mwezi, kilichofanyika ofisini kwao.
Alisema,
lazima wasaidizi hao wa sheria waelewa kuwa, wajibu wao kwa jamii, ni kuendelea
kuwahudumia kila siku na kila wakati, kwani wamekuwa wakiwategemea katika
kuapata haki zao.
Alieleza
kuwa, ndio maana CHAPO kwa kushirikiana jumuiya nyingine, imekuwa ikiwapatia
mafunzo ya kuwajengea uwezo wasaidizi hao wa sheria, ili wawe na uweledi wanapokutana
na jamii.
Mkurugenzi
huyo alifahamisha kuwa, wapo wananchi ambao wameshakata tamaa ya kupata haki
zao, hivyo ni wajibu wa wasaidizi wa sheria, kuwapa ushauri ili kutimiza ndoto
zao.
‘’Kwanza
niwashukuru kwa kazi mnayoendelea kuifanya, lakini endeleeni kukaza kamba,
katika kuwahudumia wananchi, hasa suala la kuwapa elimu na msaada wa
kisheria,’’alieleza.
Katika hatua
nyingine, Mkurugenzi huyo wa CHAPO, alisema wameshajipanga, ili kuhakikisha
wananchi wa shehia ya Wawi, kama eneo la majaribio kuwezesha kielimu.
‘’Wawi
tumeichagua kama eneo la majaribio, kwa kuanzisha darasa maalum la kuwafundisha
wanajamii sheria mbali mbali, na kisha mpango huo utaendelea kwenye shehia
nyingine,’’alieleza.
Akizungumzia
juu ya umoja na mshikamano, amewakumbusha wasadizi hao wa sheria, kuendelea
kusaidiana, kushirikiana katika shughuli zao mbali mbali, za kuwafikia
wananchi.
Mapema
Mratibu wa ‘CHAPO’ Mohamed Hassan Ali, aliwakumbusha wasaidizi wa sheria,
wanaopata mafunzo mbali mbali, kuwashirikisha na wengine.
‘’Kwa mfano,
hivi karibuni tulipata mafunzo ya mabadiliko ya sheria, sasa kama kuna wenzetu
hawakupata, lazima tuwaelekeze,’’alifafanua.
Aidha
amewahimiza wasaidizi hao wa sheria, kuhudhuria na kwa wakati, wanapokuwa na
vikao vyao ndani, kwani huwa wanamambo kadhaa ya kuyajadili.
‘’Kwanza
tupunguze utoro na dhararu, maana sisi wasaidizi wa sheria, ndio tegemeo la
wananchi wa wilaya ya Chake chake, katika eneo la utoaji wa elimu, msaada na
ushauri wa kisheria,’’alieleza.
Msaidizi wa
sheria Jimbo la Ziwani, Khadija Said Khalfan, alisema anaunga mkono wazo la
kujipangia ratiba na kuhudhuria ofisi ya ‘CHAPO’ kwa ajili ya kutoa huduma.
‘’Ni kweli,
lazima tujangie utaratibu wa kuja ofisini kila siku, ili kuwapokea wananchi ambao
wanahitaji ushauri, msaada au elimu ya kisheria,’’alipendekeza.
Nae Msaisizi
wa sheria, Jimbo la Chake chake Rikizi Hamad Ali, amesema, umoja na mshikamano
ndio ambao utepelekea ‘CHAPO’ kuwa juu kiutendaji.
‘’Tufanyeni
kazi kwa timu, ili tukienda sehemu moja kutoa elimu tunakwenda kwa wingi, kwani
wengine watapata kujifunza na wengine, kuongeza uweledi,’’alishauri.
CHAPO
imekuwa na utaratibu wa kukutana na wanachama wake kila mwisho wa mwezi, ambapo
pamoja na mambo mengine, ni kuwasilisha ripoti za mwezi za utoaji elimu na
msaada wa kisheria.
Mwisho





Comments
Post a Comment