WANANCHI DODO PEMBA WAIPA TANO CHAPO
NA HAJI NASSOR, PEMBA
WANANCHI wa shehia ya Dodo wilaya ya
Mkoani Pemba, wameipongeza Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake
‘CHAPO’ kwa uamuzi wake wa kuwafuata na kuwape elimu ya umuhimu wa upimaji wa
ardhi zao, ambao unaweza kuwa suluhu ya migogoro.
Walisema
zipo tasisi kadhaa, zimaekuwa zikijifungia ndani na kukaa na wataalamu wao
ofisini, huku wananchi wakikosa uwelewa wa mambo kadhaa, ingawa kwa ‘CHAPO’ wao
hilo hawakulibali.
Wakizungumza
kwenye mkutano wa wazi, ulioandaliwa na ‘CHAPO’ kwa kushirikiana na ‘the
foundation for civil Society na Search for Common Ground’ na kufanyika August 4, 2022 skuli ya
Dodo, walisema uamuzi huo, unafaa kuungwa mkono.
Wananachi
hao walisema, elimu ya njia ya utatuzi wa migogoro kwa njia ya amani, umuhimu
wa kusajili ardhi, utambuzi wa mipaka na kuitumia Kamisheni ya wakfu kwenye
urithi, ni mambo mema kwao.
Mmoja kati
ya wananchi hao, Faki Shaib, alisema CHAPO imefanya jambo jema, na wameona
umuhimu wa kuhudhuria mkutano huo.
‘’Kama elimu
hii ya umuhimu wa usajili wa radhi, nini maana ya ardhi kisheria, njia za
kumiliki ardhi na urithishaji kwa kutumia Kamisheni ya wakfu, twengeipata
zamani, kusingekweko migogoro ya ardhi,’’alieleza.
Nae Seif Ali
Seif alieleza kuwa, wafadhili wa CHAPO waliowawezesha kuwafikia wao Dodo,
hawakukosea uamuzi huo, na wanafurahia mano ujio wao.
Kwa upande
wake mwananchi Ali Juma Abdalla, alieleza kuwa awali walikuwa na hofu ya
kuzifikisha ardhi zao Idara ya upimaji, wakihofia gharama kubwa.
Aidha alieleza
kuwa, walikuwa hawajui kuwa, kwa sasa gharama za urithishaji kutoka Kamisheni
ya wakfu serikali imeshapunguza.
‘’Mkutano
huu wa leo, mimi umenitoa kwenye giza na sasa naishi kwenye mwanga, kuhusu
umuhimu wa kuzitumia idara za serikali, katika urithishaji au ununuzi wa ardhi,’’alieleza.
Alieleza kuwa,
lengo la mkutano huo ni kuwaelekeza wananchi athari za kila mgogoro wa ardhi
kuupeleka mahakamani, ambapo kwanza watapoteza gharama na suluhu itakuwa ngumu.
‘’Endeleeni
kuitika wito kila mnaposikia uwepo wa mikutano, maana faida zake ni kubwa, na
leo hii naamini baada ya kuwasikiliza wataalamu, mmeelewa chanzo cha migogoro
ya ardhi,’’alifafanua.
Mwakilishi huyo,
alieleza kuwa moja ya eneo ya utekelezaji wa mradi huo, ni kuwaelekeza wananchi
namna bora ya utatuzi wa migogoro kwa njia ya amani.
Alieleza kuwa,
ardhi imekuwa tishio kubwa la uwepo wa migogoro ndio, maana jumuiya ya
wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake ‘CHAPO’, imeamuwa kuwaelekeza
wananchi.
Akizungumza
na wananchi hao, Mratibu wa Kituo cha Huduma za sheria Zanzibar ‘ZLSC’ tawi la
Pemba, Safia Saleh Sultan, alisema, makosa yote ya madai, ni vyema jamii
wakayawekea vikao vya familia.
Afisa
Utambuzi wa Ardhi Pemba Faki Ali, amesema ardhi iliyotambuliwa na kupatikana
hati ya matumizi, huongeza thamani yake.
Hata hivyo
amewakumbusha wananchi kuwa, kuanza sasa mpango wa utambuzi wa ardhi zao, na
sio kusuburi ule wa serikali, ambao umeshaanza katika baadhi ya shehia.
Akighairisha
mkutano huo, sheha wa shehia ya Dodo Ramadhan Far-han Far-jala, ameipongeza
CHAPO, kwa kuamua kuwafuata na kuwapa elimu hiyo.
Jumuiya ya
wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake ambayo imeanzishwa mwaka 2016, kwa
sasa inaendelea na mradi ‘Kujenga uwelewa kwa jamii, katika kuzuia migogoro
itokanayo na matumizi ya ardhi katika shehi za Dodo, Pujini na Mfikiwa Mkoa wa
kusini Pemba.
Mwisho












Comments
Post a Comment